Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, October 30, 2009

MAGUFULI kugawa samaki Bure

Serikali imeamua kugawa bure samaki waliokamatwa kutokana na wavuvi haramu wa kimataifa kupatikana wakivua kwenye eneo la bahari ndefu kinyume cha sheria. Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, John Magufuli, alisema jana kuwa samaki hao watatolewa bila malipo kwa vyuo, shule za sekondari za bweni na hospitali. Kwa mujibu wa Magufuli, taasisi nyingine zitakazonufaika kwa mgawo wa samaki hao ni vyuo vya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Jeshi la Wananchi (JWTZ), vyuo vya uganga, taasisi za kidini zinazotoa huduma za kijamii kama vile kuwalea na kuwatunza watoto yatima na wazee. Alisema taasisi itakayohitaji samaki hao italazimika kutuma maombi kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo ama kwa Mkurugenzi wa Uvuvi. Magufuli alisema hatua ya kuwatoa samaki hao imefikiwa baada ya kupata amri ya mahakama, iliyoamuru kwamba serikali inaweza kuwauza ama kuwagawa bila malipo samaki hao. Hata hivyo, Magufuli alisema kipaumbele cha ugawaji wa samaki hao kitaelekezwa kwa taasisi zilizopo jijini Dar es Salaam, kwa kuwa wanufaika watalazimika kujigharamia gharama za usafirishaji. Magufuli alisema kwa kuwa samaki hao hawatauzwa, serikali imeweka utaratibu utakaowezesha watu watakaokiuka maelekezo hayo na kuwauza tofauti na malengo, watachukuliwa hatua za kisheria.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote