Kijana mwenye umri wa miaka 18 wa nchini Uingereza amemchanganya kimapenzi mama yake wa kambo kiasi cha kusababisha avunje ndoa yake na baba yake na kisha kutoroka naye.
Kijana mwenye umri wa miaka 18 wa nchini Uingereza ametoroka na mama yake wa kambo mwenye umri wa miaka 34 baada ya kumchanganya kimapenzi na kupelekea avunje ndoa yake.Benjamin Smith alisababisha ndoa ya baba yake, Andrew Smith na mama yake wa kambo Dawn Smith ivunjike ikiwa ni miezi michache baada ya kukutana naye kwa mara ya kwanza tangia alipomtelekeza alipokuwa mtoto miaka 17 iliyopita.Benjamin Smith alikutana na baba yake mwaka jana na alihamia kwenye nyumba yake kuanza maisha mapya akiishi na baba yake.Lakini muungano huo wa baba na mwana uligeuka kuwa chachu kwa baba wa kijana huyo.Mke wake alianza kufanya mapenzi na kijana huyo na haikuchukua muda mrefu ndoa yao ilivunjika.Kijana huyo na mama yake wa kambo walitoroka na kuhamia mji mwingine jirani wa Lincoln kuanza maisha mapya pamoja.Kutokana na kwamba Benjamin alikuwa na mojawapo ya funguo za nyumba ya baba yake, alirudi nyumbani kwa baba yake kisiri na kumuibia pesa sawa na paundi 150.Benjamin alikamatwa na polisi na kufikishwa kizimbani ambako alikiri kosa lake na kuhukumiwa kufanya kazi bila malipo kwa masaa 60 pamoja na kumrudishia baba yake pesa alizomuibia.Si baba, mwana wala mama wa kambo ambaye alikuwa tayari kuzungumzia mkasa huu ambao umewavutia watu wengi nchini Uingereza.
Kijana mwenye umri wa miaka 18 wa nchini Uingereza ametoroka na mama yake wa kambo mwenye umri wa miaka 34 baada ya kumchanganya kimapenzi na kupelekea avunje ndoa yake.Benjamin Smith alisababisha ndoa ya baba yake, Andrew Smith na mama yake wa kambo Dawn Smith ivunjike ikiwa ni miezi michache baada ya kukutana naye kwa mara ya kwanza tangia alipomtelekeza alipokuwa mtoto miaka 17 iliyopita.Benjamin Smith alikutana na baba yake mwaka jana na alihamia kwenye nyumba yake kuanza maisha mapya akiishi na baba yake.Lakini muungano huo wa baba na mwana uligeuka kuwa chachu kwa baba wa kijana huyo.Mke wake alianza kufanya mapenzi na kijana huyo na haikuchukua muda mrefu ndoa yao ilivunjika.Kijana huyo na mama yake wa kambo walitoroka na kuhamia mji mwingine jirani wa Lincoln kuanza maisha mapya pamoja.Kutokana na kwamba Benjamin alikuwa na mojawapo ya funguo za nyumba ya baba yake, alirudi nyumbani kwa baba yake kisiri na kumuibia pesa sawa na paundi 150.Benjamin alikamatwa na polisi na kufikishwa kizimbani ambako alikiri kosa lake na kuhukumiwa kufanya kazi bila malipo kwa masaa 60 pamoja na kumrudishia baba yake pesa alizomuibia.Si baba, mwana wala mama wa kambo ambaye alikuwa tayari kuzungumzia mkasa huu ambao umewavutia watu wengi nchini Uingereza.
No comments:
Post a Comment