Picha ikimuonyesha Rais Kikwete akiwa ofisini siku ya kwanza baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa 4 wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 16 Jan 2006
Rais wa Tanzania Dr. Jakaya Kikwete jana amelazimika kukatiza hotuba yake ghafla akionekana mchovu, na kuomba kuhutubia akiwa amekaa, jambo ambalo hata hivyo alilikatiza na baadaye kuondolewa kwenye jukwaa katika uwanja CCM kirumba mjini Mwanza na kwenda chumba maalum kwa ajili ya mapumziko mafupi. Hali hiyo imetokea wakati Rais Kikwete akihutubia maelfu ya waumini wa kanisa la Africa Inland Church Tanzania katika madhimisho ya miaka 100 tangu kuanzishwa kanisa hilo nchini. Rais Kikwete alikatisha hotuba yake baada ya kutojisikia vizuri huku sauti yake ikisikika kudhoofu kama mtu ambaye amepatwa na matatizo. Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu DAR ES SALAAM kwa vyombo vya habari imesema Rais Kikwete alilazimika kupumzika kutokana na kuzidiwa na uchovu kufuatia shughuli nyingi mfululizo katika siku za karibuni. Hata hivyo baada ya mapumziko ya muda aliendelea kushiriki katika shughuli hizo hadi mwisho.
“Nguvu imerudi…napenda sasa kuchukua nafasi hii kuzindua rasmi uchangiaji wa shughuli za Kanisa lenu na mimi naanza na mchango wa sh. 1,000,000,” Rais Kikwete aliwaambia maelfu ya waumini wa AICT huku wakimshangilia kwa nguvu mara aliporejea jukwaani. Pia Rais alisema “Kwa kweli mshituko huu wa leo ni matokeo ya ubishi wangu. Nilishauriwa na wasaidizi wangu nipumzike baada ya kurejea nyumbani kutoka Marekani. Niliambiwa nisiende Arusha ama kuja hapa. Lakini nikakataa. Siku nyingine nitawasiliza zaidi.”
Rais wa Tanzania Dr. Jakaya Kikwete jana amelazimika kukatiza hotuba yake ghafla akionekana mchovu, na kuomba kuhutubia akiwa amekaa, jambo ambalo hata hivyo alilikatiza na baadaye kuondolewa kwenye jukwaa katika uwanja CCM kirumba mjini Mwanza na kwenda chumba maalum kwa ajili ya mapumziko mafupi. Hali hiyo imetokea wakati Rais Kikwete akihutubia maelfu ya waumini wa kanisa la Africa Inland Church Tanzania katika madhimisho ya miaka 100 tangu kuanzishwa kanisa hilo nchini. Rais Kikwete alikatisha hotuba yake baada ya kutojisikia vizuri huku sauti yake ikisikika kudhoofu kama mtu ambaye amepatwa na matatizo. Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu DAR ES SALAAM kwa vyombo vya habari imesema Rais Kikwete alilazimika kupumzika kutokana na kuzidiwa na uchovu kufuatia shughuli nyingi mfululizo katika siku za karibuni. Hata hivyo baada ya mapumziko ya muda aliendelea kushiriki katika shughuli hizo hadi mwisho.
“Nguvu imerudi…napenda sasa kuchukua nafasi hii kuzindua rasmi uchangiaji wa shughuli za Kanisa lenu na mimi naanza na mchango wa sh. 1,000,000,” Rais Kikwete aliwaambia maelfu ya waumini wa AICT huku wakimshangilia kwa nguvu mara aliporejea jukwaani. Pia Rais alisema “Kwa kweli mshituko huu wa leo ni matokeo ya ubishi wangu. Nilishauriwa na wasaidizi wangu nipumzike baada ya kurejea nyumbani kutoka Marekani. Niliambiwa nisiende Arusha ama kuja hapa. Lakini nikakataa. Siku nyingine nitawasiliza zaidi.”
No comments:
Post a Comment