Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, October 30, 2009

FIFA & TFF kuzindua Program ya kuimarisha SOKA

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) kwa kushirikiana na lile la kimataifa, Fifa wamezindua programu maalum ya soka ya watoto kati ya miaka 6-12 ambayo itaanza hivi karibuni nchini kote. Lengo la kuanzisha programu hiyo nchini ni kutaka soka la watoto liweze kukua na kufika mbali pamoja na kupata wachezaji bora ambao wataiowakilisha nchi baadae katika mashindano mbalimbali. Rais wa TFF, Leordegar Tenga alisema jana kuwa waliomba mradi huo toka Fifa na wamekubali kwa kufuata kanuni zake hivyo kuwataka watoto wengi wajitokeze. Alisema walikutana na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo na Mkurugenzi wa Fifa kwa nchi za Afrika, Ashford Mamelodi na kukubaliana jinsi ya kuendesha programu hiyo nchi nzima pamoja na kupata wadhamini. "Tayari tumekutana na wahusika mara baada ya kupata kibali kutoka Fifa na wamekubalina hivyo kwa sasa wako katika mchakato wa kupata wadhamini watakaowasaidia kuendesha mradi huo,"alisema Tenga. Mkurugenzi wa Fifa, Ashford Mamelodi alisema wamezindua programu hiyo nchini kote ambayo itashirikisha jinsia zote na wamefurahishwa na serikali kwa kuonyesha moyo wa kuwasaidia. Alisema Fifa watasaidia katika mashindano mbalimbali watakayoandaa pamoja na kufundisha walimu vifaa mbalimbali ambavyo vitahitajika na kuwataka TFF kuwa makini katika kuendeleza hilo. "Lazima tuanzie ngazi za chini tukitaka kufika mbali kisoka kwani hakuna njia mbadala ya kufika mafanikio makubwa bila njia hizo",alisema Mamelodi.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote