Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, October 12, 2009

Je Wajua kama Zombe aachia ngazi jeshi la Polisi?


ALIYEKUWA Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe ameandika barua ya kuacha kazi katika jeshi hilo baada ya Serikali kukata dhidi yake. Jeshi la Polisi limethibitisha kupokea barua ya Zombe inayoeleza kutotaka tena kuendelea na ajira ya jeshi hilo.Maamuzi ya Zombe yamekuja kwa kudai kuwa baada ya kuona amefikia hatua hiyo ya hofu ya kwa kutengenezewa kesi nyingine na kulazimika kuandika barua ya kuomba kuacha kazi.Kamishna wa utawala na rasilimali watu wa Jeshi la Polisi, CP Clodwig Mtweve, amesema barua hiyo imepokelewa na imekabidhiwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ambaye kiutaratibu ndiye mwajiri wa Zombe.Mtwere alisema kuwa katibu huyo ndiye mwenye mamlaka ya kujibu barua hiyo ya kuacha kazi ama kuendelea nay eye ndiye atakayekuwa na mamlaka juu ya maombi hayo.Hatua ya Zombe imekuja baada Juzi Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) alikata rufani dhidi ya Zombe na wenzake wanaotuhumiwa kwa mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro, na dereva teksi mmoja.Rufani hiyo ina sababu 11 zinazopinga kuachiwa huru kwa washitakiwa hao wanaodaiwa kuwaua kwa makusudi wafanyabiashara hao.Sababu hizo zilizowasilishwa na DPP ni pamoja na Jaji Salum Massati, ambaye ndiye alikuwa akisikiliza kesi hiyo na kutoa hukumu ya kuwaachia huru washitakiwa hao, kufanya makosa katika kujielekeza, kujenga na kutoa tafsiri katika kanuni za kosa.Rufani hiyo inadai kuwa Jaji Massati alifanya makosa katika kumwachia huru mshitakiwa wa kwanza, ambaye ni Zombe, pamoja na kuwapo ushahidi wa kutosha wa kimazingira ambao ungeweza kumtia hatiani.Rufani hiyo pia inadai kuwa Jaji alishindwa kutoa sababu za washitakiwa wa WP Jane na D.2300 D/CPL Sarro kwa kuathirika kwao kimazingira kama alivyoeleza kwenye hukumu yake.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote