Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, October 30, 2009

Habari Njema Kwa Matasa

Wapenzi ambao hawana uwezo wa kupata mtoto kutokana na mmoja wao kuwa tasa, watapata nafasi ya kuwa na watoto kufuatia ugunduzi mpya wa wanasayansi ambapo mtoto atatengenezwa kwenye maabara kutokana na mbegu za kiume na mayai ya uzazi ya mwanamke vyote vya kutengeneza kwenye maabara. Wanasayansi nchini Marekani wako njiani kutengeneza watoto kwenye maabara baada ya kufanikiwa kutengeneza mayai ya uzazi ya mwanamke na mbegu za kiume kwenye maabara kwa kutumia mchanganyiko wa vitamini kwenye damu na kemikali mbalimbali.Mbegu za kiume na mayai ya uzazi ya mwanamke yatatengenezwa kwenye maabara bila kuhitajika kuwepo kwa mwanamke wala mwanaume.Ugunduzi huu umeshangiliwa sehemu nyingi duniani wakati ambao wanasayansi wako kwenye hatua za mwisho za kujaribu kutengeneza mtoto mwenye afya njema kutokana na mbegu za kiume na mayai ya kike vyote vya kutengeneza kwenye maabara.Ugunduzi huu utawapa nafasi watu ambao ni tasa na hawawezi kupata watoto au wale waliopoteza uwezo wa kupata mtoto kutokana na matibabu ya kansa, waweze kupata watoto kutokana na damu zao.Serikali ya Marekani ndiyo iliyodhamini utafiti huo uliofanyika kwenye chuo kikuu cha Stanford University ambapo wanasayansi walitumia mchanganyiko wa kemikali na vitamini kuweza kutengeneza seli ambazo baadae zitatumika kutengeneza mayai ya kike na mbegu za kiume.Wanasayansi hao walisema kuwa lengo kubwa lililopo hivi sasa ni kujaribu kujaribu kupata mtoto mwenye afya njema kwenye maabara.

1 comment:

Anonymous said...

mmmh hawa wanasayansi sasa!!!!!!!!! haya tunasubiri

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote