Safari yake ya Muziki
Pipi alianza Muziki kwenye miaka ya mwaka 2004 akiwa anasoma
kidato cha kwanza, na mgunduzi wa kipaji chake ni mama yake
mzazi aliyekuwa akimpata moyo baada ya kumsikia akiimba nyimbo
mbalimbali za wanamuziki wa nje kama Celion Dion na Kelly Clerkosn.
Album
Kuhusu Album binafsi hadi sasa Pipi hajafanikiwa kutoa ila binafsi
anasema hilo wazo lipo na muda ukifika ataingia uwanjani.
Anaongeleaje kuhusu Muziki wa Tanzania
Kwa sasa muziki wa Kitanzania unapanda chati kwa sana
ila haulipi sana, anadai Promota wanabana ila ana imani ipo
siku wataachia
Wanamuziki anaowapenda
Kwa Tanzania anamzimia sana Nakaaya na Barnaba na kwa
nje ya nchi Alicia Keys na Lil Wayne.
Shughuli nje ya Muziki
Anasoma Chuo
Mahusiano
Kwa sasa hana
Pipi anawashukuru washabiki wake wote kwa kumpokea kwa mikono miwili anasema hakutegemea kama ingejulikana hivi amekubalika na kupendwa sana ingawa wimbo haukuwa wake alishirikishwa tu na Barnaba , Pia aliwaasa wasanii chipukizi wawe macho na mafataki kwani wakishajuwa unajina watakufuatia sana . Pipi katoa shukrani za pekee kwa Mungu kwa kila kitu, mashabiki wake wote, THT bila kumsahau mama yake kipenzi na familia yake kwa kuwa nae wakati wote.
No comments:
Post a Comment