Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, October 28, 2009

Waaga Dunia wakijaribu kumuokoa mwenzao


WATU wawili: Pili Daud (29) na Amina Masud (44) wakazi wa Kawe Ukwamani, jijini Dar es Salaam, wamefariki dunia wakati wa harakati za kumuokoa Mariam Mwinyimvua (65) aliyekuwa amenaswa na umeme. Mariamu bado ni majeruhi huku wale waliotaka kumuokoa wakiwa wameaga dunia! Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya asubuhi, katika eneo hilo wakati Mariam Mwinyimvua (65) alipokuwa akitaka kuanika nguo katika kamba. Kwa mujibu wa Kamanda Kalunguyeye, kifo cha watu hao kilitokea baada ya Mariam Mwinyimvua kufua nguo zake na kuzianika kwenye waya wa umeme na kusababisha kunaswa ghafla. Kwa mujibu wa kamanda huyo, baada ya Mariam kunaswa ndipo Pili Daud alitokea kwa lengo la kumuokoa katika ajali hiyo na kwamba wakati akiwa kwenye harakati hizo naye alinaswa na umeme na kufariki papo hapo. Alisema baadaye alitokea Amina Masoud kwa lengo la kutoa msaada kwa wote wawili naye alinaswa pia na kufa papo hapo! “Walikufa wote wawili wakiwa katika harakati za kumuokoa ndugu yao aliyenaswa wakati akianika nguo,” alisema Kalunguyeye. Baada ya kutokea hali hiyo, Jeshi la Polisi, kwa kusaidiana na majirani, lilifanikiwa kumpa huduma ya kwanza Mwinyimvua na kisha kumkimbiza katika Hospitali ya Mwananyamala. Halikadhalika maiti za Pili na Amina zilipelekwa hospitalini hapo. Tanzania Daima Jumatano, ilipowasiliana na Kamanda Kalunguyeye baadaye kwa njia ya simu, alisema kuwa hali ya majeruhi huyo ni mbaya na wamemhamishia katika chumba cha wagonjwa mahututi.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote