Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, October 15, 2009

Mzee wa Mavocal aondoka na Milioni 25

Hatimaye kile kitendawili cha nani atajiondokea na mzigo mzima wa Tsh 25,000,000/- za kitanzania ulitatuliwa usiku wa juzi pale katika ukumbi wa Diamond Jubilee mara baada ya Pascal Cassian a.k.a Mzee wa Vocal au BabaRita kuondoka na kitita hicho. Diamond Jubilee ilifurika kiasi cha kukosa nafasi ya kupitisha mguu pale washabiki wengi walipojitokeza kushuhudia fainali hiyo ambayo ilirushwa Live katika mtando wa Dar411 na kituo cha televisheni cha ITV. Kabla ya kuanza kwa fainali Chief Judge Madame Rita alipanda jukwaani kutoa shukrani zake kwa wote waliofanikisha kwa namna moja au nyingine kuweza kuifikisha Bongo Star Search katika fainali hiyo. alitoa shukrani kwa wadhamini wakuu ambao ni Vodacom Tanzania, Kilimanjaro na wengine wote waliofanikisha toka mwanzo wa safari mpaka hapa tulipofika, bila kuwasahau wafanyakazi wote wa Benchamark”

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote