Katika kuwapa ahueni wateja wake kimawasiliano katika wakati ambao teknolojia imekua, Kampuni ya simu za mikononi ya Zain imeleta tena huduma mpya ijulikanayo kama Pamoja Plus (+) itakayoanza kufanya kazi kuanzia sasa.
Akifanya uzinduzi huo jana asubuhi kwenye ukumbi wa Kibo katika Hoteli ya Kilimanjaro (Kempinski) hapa Dar es Salaam mbele ya Wanahabari, Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania Bwana Khaled Muhtadi amesema kwa sasa wateja wake watapata huduma nafuu kwa kupewa punguzo la hadi asilimia hamsini (50%) kwa simu za Zain pamoja na mitandao mingine watakazopiga. Ameeleza kuwa mteja atakayejiunga na huduma hiyo (Pamoja Plus), atapata nafasi ya kusajili namba za watu kumi (10) wa mtandao wa Zain atakazopata, kisha ataongeza tena namba moja kutoka mtandao mwingine wowote aupendao ambayo nayo itafaidi punguzo hilo huku akiweza kubadilibadili namba hizo hadi mara tatu kwa mwezi apendavyo. Aidha Mkurugenzi huyo Mtendaji wa Zain nchini amesema zile simu za Zain zitakazopigwa na ambazo haziko katika chaguo la namba alizozisajili katika Pamoja Plus nazo zitapata punguzo la asilimia ishirini (20%) na pia zile za mitandao mingine ambazo nazo hazijasajiliwa zitapata punguzo la asilimia kumi na saba (17%).
Akifanya uzinduzi huo jana asubuhi kwenye ukumbi wa Kibo katika Hoteli ya Kilimanjaro (Kempinski) hapa Dar es Salaam mbele ya Wanahabari, Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania Bwana Khaled Muhtadi amesema kwa sasa wateja wake watapata huduma nafuu kwa kupewa punguzo la hadi asilimia hamsini (50%) kwa simu za Zain pamoja na mitandao mingine watakazopiga. Ameeleza kuwa mteja atakayejiunga na huduma hiyo (Pamoja Plus), atapata nafasi ya kusajili namba za watu kumi (10) wa mtandao wa Zain atakazopata, kisha ataongeza tena namba moja kutoka mtandao mwingine wowote aupendao ambayo nayo itafaidi punguzo hilo huku akiweza kubadilibadili namba hizo hadi mara tatu kwa mwezi apendavyo. Aidha Mkurugenzi huyo Mtendaji wa Zain nchini amesema zile simu za Zain zitakazopigwa na ambazo haziko katika chaguo la namba alizozisajili katika Pamoja Plus nazo zitapata punguzo la asilimia ishirini (20%) na pia zile za mitandao mingine ambazo nazo hazijasajiliwa zitapata punguzo la asilimia kumi na saba (17%).
No comments:
Post a Comment