Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, October 30, 2009

Kesi ya EPA yaahirishwa hadi Mwakani

UGONJWA wa mshtakiwa Farijara Hussein umekwamisha kuendelea kusikilizwa kwa kesi ya wizi wa Sh 3.8 bilioni za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) inayomkabili yeye pamoja na wenzake watano na sasa kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mwakani ili kutoa nafasi ya mtuhumiwa huyo kupata matibabu. Kesi hiyo ilishindwa kuendelea kusikilizwa jana mbele ya jopo la mahakimu watatu lililokuwa likiongozwa na Hakimu Samuel Kalua mara baada ya Wakili wa Serikali, Oswald Tibabyekomya kudai kuwa wapo tayari kwa ajili ya kuendelea kuisikiliza na kwamba wana mashahidi wawili. Baada ya maelezo hayo, Wakili Majura Magafu anayemtetea mshtakiwa Farijara, aliiomba mahakama iahirishe kesi hiyo kwa sababu mteja wake huyo anaumwa na amepewa muda wa mampuziko wa siku tatu (ED) kuanzia juzi, jana na leo. Magafu aliendelea kudai mbali na mapumziko hayo pia alitakiwa aonane na mtaalamu wa hospitali ya Burhan, Profesa Aboud. Kufuatia hoja hiyo hakimu Kalua alikubaliana na maombi hayo na kuiahirisha kesi hiyo hadi Novemba 11, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na si kuendelea kusikilizwa ambapo alisema kuwa Desemba 21, mwaka huu kesi hiyo itatajwa tena na kuongeza kuwa kuanzia Februari Mosi hadi 5, 2010 kesi hiyo ndio itaendelea kusikilizwa mfululizo. Awali Oktoba 27 mwaka huu, mahakama ililazimika kusimama kusikiliza ushahidi katika kesi hiyo baada ya mshtakiwa huyo kuomba kwenda haja ndogo mara kwa mara kutokana na kusumbuliwa na tatizo la figo. Mshtakiwa huyo aliomba kwenda haja ndogo mara kwa mara na kusababisha hakimu kuamua kumruhusu aondoke. Akitoa ushahidi wake Msajili Msaidizi kutoka ofisi ya Msajili wa Majina ya Biashara na Kampuni (Brela), Rehema Kitambi alidai kuwa mshtakiwa Farijara na mtu mwingine aliyemtaja kwa jina la Kiza Selemani walighushi jina la biashara la Mibale Farm lililotumika kuchota fedha hizo za EPA. Alidai kuwa hati zenye jina la Mibale Farm hazitambui kwasababu hazijatolewa na Brela na hata saini inayoonekana katika baadhi ya hati hizo imeghushiwa na kufanana na ya kwake. Shahidi huyo alidai kuwa Septemba 2 mwaka 2005 Farijara na Kiza waliomba kusajili jina la biashara la Nibale Farm na kwamba Septemba 5 mwaka 2005 walipeleka maombi mengine ya kubadili jina hilo ili liwe Mibale Farm. Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Rajabu Maranda, Ajay Somani, Imani Mwaposya, Ester Komu na Sophia Kalika. Washtakiwa hao wanadaiwa kuiibia BoT Sh 3.8 bilioni baada ya kudanganya kuwa kampuni ya Mibale Farm imepewa deni na kampuni ya Lakshmi Textile Mills ya nchini India.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote