Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, October 26, 2009

Je tutafika? Malawi Yajiandaa Kuhalalisha Uhakaba

Serikali ya Malawi inajiandaa kupitisha sheria itakayohalalisha biashara ya ukahaba nchini humo kwa kuwaruhusu makahaba wafanye ukahaba kwenye majumba yao badala ya kusimama barabarani. hatua hiyo ya serikali ya Malawi inakusudia kuwalinda wanawake wanaojiuza barabarani kutokana na manyanyaso wanayopata kutoka kwa wateja wao.Waziri wa masuala ya jamii na maendeleo wa Malawi, bi Patricia Kaliati akiongea na shirika la habari la Reuters alisema kwamba muswada wa kuruhusu biashara ya ukahaba majumbani nchini humo uko kwenye hatua za mwisho kupelekwa bungeni ili upitishwe uwe sheria."Tunataka watoke mitaani wakafurahie tendo la ngono kwenye majumba yao na hivyo kuepukana na kunyanyaswa kijinsia au kubakwa na wateja wao na hivyo kuwalinda na gonjwa la ukimwi", alisema Kaliati.Ugonjwa wa ukimwi nchini Malawi yenye idadi ya watu milioni 13 umeishaua zaidi ya watu laki nane tangia ulipoingia nchini humo mwaka 1985.Jitihada za kuwaelimisha watu kujikinga na ugonjwa huo zimesaidia kupunguza idadi ya waathirika toka asilimia 14 hadi 13. Madawa mengi yanayotolewa bure kwa waathirika yamesaidia kupunguza idadi ya vifo vya waathirika kwa asilimia 70.Hata hivyo muswada huo wa kuhalalisha ukahaba tayari umeishakumbwa na upinzani toka taasisi mbali mbali.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote