Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, October 26, 2009

Wanachama wa DECI Arusha wafungua kesi ya Madai

WANACHAMA 300 wa Kampuni ya Development Entrepreneurship Community Initiative (DECI) mkoani Arusha, wamefungua kesi ya madai katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, kudai fidia ya sh bilioni 2. Kesi hiyo inatarajiwa kuanza kutajwa rasmi leo mahakamani hapo kwa mahakama kupanga rasmi tarehe ya kuanza kusikilizwa. Wanachama hao wanaowakilisha wenzao 4,700 katika kesi hiyo, wanataka viongozi wakuu wa kampuni hiyo kuwalipa fedha zao walizopanda na riba baada ya kuvunja mkataba baina yao. Akizungumza kwa niaba ya wananchama wenzake, msemaji wa wana DECI hao, Leonard Kilasi, alisema wameamua kufungua kesi hiyo baada ya kujiridhisha kuwa viongozi wa kampuni hiyo hawana mpango wa kurejesha fedha zao. “Mpaka sasa hatufahamu hatma ya fedha zetu, hivyo tumeamua kufungua kesi ili mahakama iweze kutenda haki na sisi tupate fedha zetu tulizopanda kabla ya kampuni hiyo kufutwa,” alisema Kilasi. Aidha, Kilasi alisema wadaiwa wa kwanza katika kesi hiyo ni wakurugenzi wa DECI makao makuu, na mwakilishi wao mkoani hapa, Salome Ilungu. Hata hivyo, wakati wana DECI hao wakikusudia kufungua kesi, tayari wakurugenzi wa taasisi hiyo inayojishughulisha na kazi ya kupanda na kuvuna pesa, wameshafunguliwa kesi na serikali wakidaiwa kuendesha mchezo huo wa upatu kinyume cha sheria.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote