Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, October 26, 2009

Hatimaye Mtoto amzaa mtoto mwenzie

Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 11 wa nchini Bulgaria ambaye jina lake liliwekwa kapuni amepata mtoto mwenzie baada ya kujifungua salama mtoto wa kike usiku wa siku ya alhamisi kwenye hospitali moja iliyopo kwenye mji wa kusini mashariki mwa Bulgaria wa Sliven.Taarifa za kujifungua kwa mtoto huyo zimethibitishwa na mganga mkuu wa wadi ya wazazi katika hospitali ya Sliven Hospital, Dr. Sonya Mihaylova, ambaye alisema awali katika hospitali hiyo hiyo mtoto mwingine mwenye umri wa miaka 12 aliwahi kujifungua mtoto.Mama huyo mtoto mwenye umri wa miaka 11 alijifungua mtoto mwenye afya njema mwenye uzito wa kilo 2.5.Alijifungua mtoto huyo baada ya kupewa mimba na kijana mwenye umri wa miaka 19 ambaye jina lake nalo halikutajwa.Wazazi wa binti huyo wako wanaishi nchini Hispania na binti huyo alikuwa akilelewa na mama wa kijana aliyempa ujauzito huo.Binti huyo aliingia leba saa tatu na nusu usiku na alijifungua ndani ya lisaa lisaa limoja na hapo hapo alitaka kuondoka kurudi nyumbani kwake kwakuwa harusi yake na baba wa mtoto wake ilikuwa ikifanyika usiku huo huo."Baada ya kujifungua tu alitaka kuondoka kwakuwa harusi yake ilikuwa usiku huo huo", alisema Dr. Mihaylova.“Kulikuwa hakuna ndugu yoyote toka familia yake na hakuna mtu yoyote ambaye tungeweza kumshauri chochote, wazazi wake wako Hispania na hakuna mtu anayeweza kumualia jambo zaidi ya kujiamulia mwenyewe anavyotaka", alisema Dr. Mihaylova.Dr. Mihaylova alikataa kumruhusu binti huyo aondoke mpaka atakapohakikisha binti huyo na mtoto wake wote wapo kwenye afya njema.Taarifa zaidi zilisema kwamba hospitali hiyo imetoa taarifa ya tukio hilo kwa taasisi ya kutetea haki za watoto.Waendesha mashtaka walisema wanalifanyia uchunguzi suala hilo kabla ya kutoa uamuzi kwani kufanya mapenzi na watoto wenye umri mdogo ni kosa la jinai nchini humo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote