Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, October 22, 2009

Mbwa huyu amponza Boss wake

Mwanamke mmoja mkware wa nchini Italia amefumaniwa akila uroda na mmiliki wa baa baada ya mumewe kumuona mbwa wake akiwa amefungwa nje ya eneo la tukio. Mwanamke huyo ambaye hakutajwa jina lake mwenye umri wa miaka 35 alimuaga mumewe kuwa anaenda nje kumtembeza mbwa wake na atakutana na rafiki zake kwenye kibanda cha kahawa na atarudi nyumbani baada ya masaa machache.Mumewe mwenye umri wa miaka 40 na yeye pia aliamua kuwatembeza nje watoto wao wawili wadogo na ndipo aliposhangaa kumuona mbwa wa mkewe akiwa amefungwa kwenye nguzo ya taa ya barabarani pembeni ya baa moja katika mji wao.Mbwa huyo kwa furaha alibweka na kuruka ruka alipomuona mume wa mwanamke huyo.Mume huyo aliamua kuingia kwenye baa hiyo kumsaka mkewe na ndipo alipomfumania mkewe akila uroda na mmiliki wa baa hiyo.Katika tukio hilo lililotokea kwenye mji wa Caltanissetta, Sicily, mwanaume huyo aliingia kwenye mzozo mkubwa sana na mkewe kabla ya kumshushia kipigo cha nguvu mwanaume aliyekuwa akimla uroda mkewe.Polisi waliitwa kuamua ugomvi huo na mmiliki wa baa hiyo alipelekwa hospitali akiwa ameharibiwa sura yake kwa mkong'oto aliopewa.Polisi walisema kwamba hakuna hatua yoyote waliyoichukua dhidi ya mwanaume aliyempiga mmiliki wa baa hiyo kwa kumchukulia mkewe. Hadi tunaingia Mitamboni inasemekena Mume huyo ameamua kuwasiliana na wanasheria wake na ameamua kumuacha mke huyo mkware.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote