Mapacha wa nchini India walioungana kuanzia kiunoni wenye miguu mitatu ambao wamejipatia umaarufu duniani kwa kucheza sarakasi kiasi cha kufananishwa na Buibui wamekataa ushauri wa daktari wa Marekani anayetaka kuwatenganisha ili kila mmoja ajitegemee.
Mapacha wa nchini India, Ganga na Jamuna Mondal wenye umri wa miaka 39 maarufu duniani kama "Spider Sisters" wameungana katika namna ambayo ni nadra sana kutokea duniani kwani wameungana kuanzia kiunoni lakini kila mmoja ana mguu wake mmoja huku miguu yao ya pili imeungana pamoja na kufanya mguu mmoja wa tatu wenye vidole tisa.Awali madaktari walionya kuwa kujaribu kuwatenganisha kutahatarisha maisha yao lakini daktari mtaalamu wa mapacha walioungana wa nchini Marekani, Dr James Stein aliwafanyia uchunguzi mapacha hao na amedai kuwa mapacha hao wanaweza kutenganishwa bila kuhatarisha maisha yao.Lakini mapacha hao wamekataa kutenganishwa na kusema "Tutaishi kama jinsi ambavyo Mungu ametuumba".Kila pacha mmoja ana kichwa chake na mikono yake miwili.
Mapacha wa nchini India, Ganga na Jamuna Mondal wenye umri wa miaka 39 maarufu duniani kama "Spider Sisters" wameungana katika namna ambayo ni nadra sana kutokea duniani kwani wameungana kuanzia kiunoni lakini kila mmoja ana mguu wake mmoja huku miguu yao ya pili imeungana pamoja na kufanya mguu mmoja wa tatu wenye vidole tisa.Awali madaktari walionya kuwa kujaribu kuwatenganisha kutahatarisha maisha yao lakini daktari mtaalamu wa mapacha walioungana wa nchini Marekani, Dr James Stein aliwafanyia uchunguzi mapacha hao na amedai kuwa mapacha hao wanaweza kutenganishwa bila kuhatarisha maisha yao.Lakini mapacha hao wamekataa kutenganishwa na kusema "Tutaishi kama jinsi ambavyo Mungu ametuumba".Kila pacha mmoja ana kichwa chake na mikono yake miwili.
No comments:
Post a Comment