Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, October 27, 2009

Historia kuibeba simba Jumamosi

SIMBA inayojiandaa kuikabili Yanga mwisho wa wiki katika mchezo mgumu wa Ligi Kuu ya Vodacom imeweka rekodi ya kushinda mechi tisa kati ya tisa katika mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo.Kwa mujibu wa gazeti moja la kila siku, Ikilinganishwa na watani zao, Yanga, wao bado hali si nzuri tofauti na misimu miwili iliyopita ambayo walitwaa ubingwa wakiwa chini ya mtaalam Dusan Kondic aliyeondoka.Timu hizo zinakutana Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Simba inashikilia usukani wa ligi kwa pointi 27 ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 18 sawa na Mtibwa Sugar , lakini zikiwa na tofauti ya mabao na Azam ya nne.Vijana hao wa Mzambia Patrick Phiri watajitangazia ubingwa wao wa majira ya joto na kujiweka kwenye nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa ligi msimu huu kama watapata ushindi kwenye mechi mbili za mwisho dhidi ya wapinzani wake kwenye kinyang'anyiro cha taji hilo, Yanga na Mtibwa Sugar.Mabingwa watetezi, Yanga pamoja na ushindi wao wa bao 1-0 dhidi ya Moro United mwishoni mwa wiki bado wanajua kuwa wanahitaji ushindi kwenye mechi yake ijayo ili kurudisha matumaini yake kwa kufikisha pointi 24 wakati Simba wao watamaliza ligi hiyo kwa kushinda mechi zao mbili zilizosalia watakuwa na pointi 33.Endapo wataishinda Yanga na baadaye Mtibwa, Wekundu wa Msimbazi watakuwa wamezidi kuwawashia indiketa wapinzani hao ambao itabidi wafanye kazi ya ziada kuwashusha kileleni kwenye mzunguko wa pili wa ligi utakaoanza Januari mwakani.Kwa upande wao, Yanga ambayo walianza kwa kusuasua, tayari imecheza mechi tisa imeshinda tano, imetoka sare tatu na kupoteza mchezo mmoja dhidi ya Majimaji ya Songea bado wanacho kibarua kigumu cha kubaki nafasi ya pili kutokana na upinzani mkali kutoka kwa Azam na Mtibwa Sugar.Azam inayofundishwa na Mbrazili Amourin Itamaar wameonekana kuwa na kasi kubwa ya kuwania nafasi mbili za juu huku mshambuliaji wao, John Boko , maarufu Adebayor akishikilia rekodi ya kufunga mabao manane katika mechi tisa za msimu huu.Vijana wa Manungu, Mtibwa Sugar pamoja na kuwapoteza nyota wake kadhaa msimu huu, Salum Sued, Uhuru Seleman, Zahoro Pazi, waliohamia klabu nyingine bado wameendelea kuonyesha kiwango cha juu na sasa wanashikilia nafasi ya tatu sambasamba na Yanga wakitofautiana kwa mabao ya kushinda.Wakati mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo unaeleka mwishoni Novemba 11, vita nyingine ipo kwa timu za mkiani zinazosaka kujinasua, ambazo ni Prisons ya Mbeya, African Lyon na Toto Africa ya Mwanza na JKT Ruvu (Pwani), zote zipo kwenye hati hati ya kushuka daraja iwapo hazitabadilika mwenendo wao kwenye mzunguko wa pili wa ligi hiyo, kati ya hizo zitajikuta ligi daraja la kwanza.Prisons ambayo ni ya 10 katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi nane tayari imecheza michezo tisa, ikifuatiwa na Lyon yenye pointi saba huku Toto inashika mkia kwa pointi nne, kabla ya mechi ya jana.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote