Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, October 21, 2009

Huu ni Ukatili kupitiliza ukomeshwe

JESHI la polisi mkoani Mwanza, limefanikiwa kuipata mifupa ya albino kufuatia kumtia mbaroni mtuhumiwa wa kesi ya mauaji, aliyekuwa akisakwa tangu Juni mwaka huu.Kukamatwa kwake kumesaidia kupatikana kwa ushahidi wa mifupa ya marehemu, Jesca Charles iliyokuwa imefichwa kichakani baada ya kuuawa Juni 21 mwaka huu.Akizungumza na waandishi wa habari jana Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Elias Kalinga alisema kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo (jina linahifadhiwa) kuliwezesha kupatikana kwa mifupa sita ya miguu na mikono ya marehemu Jesca.Kalinga alisema kukamatwa kwa mtuhumiwa kulitokana na maendeleo ya upelelezi wa kesi ya mauaji namba 28/2009 ya Jesca Charles aliyeuawa kwa kukatwa mapanga mikono na miguu Igoma jijini Mwanza na wauaji wake kutoweka na baadhi ya viungo vyake.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote