Mlowezi wa kizungu aliyemuua kwa kumpiga risasi raia wa Kenya aliyeingia kwenye shamba lake na baadae kutupwa jela miezi minane ameachiliwa huru kabla ya kumaliza kifungo chake baada ya kuonyesha tabia nzuri.
Mlowezi Tom Cholmondeley alihukumiwa kwenda jela miezi minane baada ya kesi yake ya mauaji kubadilishwa kuwa kesi ya kuua bila kukusudia.Mlowezi huyo tajiri alimuua kwa kumpiga risasi raia wa Kenya, Robert Njoya aliyeingia kwenye shamba lake lililopo kwenye mkoa wa Rift Valley ili kuwinda wanyama pori.Mlowezi huyo aliachiwa huru ijumaa kabla ya hata ya miezi minane aliyohukumiwa kuisha kwa kile kilichoelezwa kuwa alionyesha tabia nzuri.Wakati alipokuhumiwa kutumikia kifungo cha miezi minane jela mwezi wa tano mwaka huu, mlowezi huyo alikuwa ameishakaa jela miaka mitatu akisubiria hukumu yake.Jaji wa mahakama kuu ya Kenya, Muga Apondi ndiye aliyetoa hukumu hiyo ya miezi minane jela na kusababisha hasira za wananchi mbali mbali wa Kenya waliokuwa wakilalamika kuwa sheria imepindishwa ili kuwabeba matajiri.Jaji Apondi akiielezea hukumu aliyoitoa alisema kuwa mlowezi huyo hakuua kwa kukusudia kwani baada ya kumpiga risasi Robert Njoya, alijaribu kutoa huduma ya kwanza na alimpeleka hospitali.Mwaka mmoja kabla ya kumuua Robert Njoya mlowezi huyo huyo alimuua raia mwingine wa Kenya lakini kesi yake ilifutwa katika hali ya utatanishi.
Mlowezi Tom Cholmondeley alihukumiwa kwenda jela miezi minane baada ya kesi yake ya mauaji kubadilishwa kuwa kesi ya kuua bila kukusudia.Mlowezi huyo tajiri alimuua kwa kumpiga risasi raia wa Kenya, Robert Njoya aliyeingia kwenye shamba lake lililopo kwenye mkoa wa Rift Valley ili kuwinda wanyama pori.Mlowezi huyo aliachiwa huru ijumaa kabla ya hata ya miezi minane aliyohukumiwa kuisha kwa kile kilichoelezwa kuwa alionyesha tabia nzuri.Wakati alipokuhumiwa kutumikia kifungo cha miezi minane jela mwezi wa tano mwaka huu, mlowezi huyo alikuwa ameishakaa jela miaka mitatu akisubiria hukumu yake.Jaji wa mahakama kuu ya Kenya, Muga Apondi ndiye aliyetoa hukumu hiyo ya miezi minane jela na kusababisha hasira za wananchi mbali mbali wa Kenya waliokuwa wakilalamika kuwa sheria imepindishwa ili kuwabeba matajiri.Jaji Apondi akiielezea hukumu aliyoitoa alisema kuwa mlowezi huyo hakuua kwa kukusudia kwani baada ya kumpiga risasi Robert Njoya, alijaribu kutoa huduma ya kwanza na alimpeleka hospitali.Mwaka mmoja kabla ya kumuua Robert Njoya mlowezi huyo huyo alimuua raia mwingine wa Kenya lakini kesi yake ilifutwa katika hali ya utatanishi.
No comments:
Post a Comment