Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, October 26, 2009

Je haki imetendeka? Ahukumiwa kifungo cha miezi 8 kwa kosa la Mauaji na kuachiwa huku baada ya kutumikia miezi 3

Mlowezi wa kizungu aliyemuua kwa kumpiga risasi raia wa Kenya aliyeingia kwenye shamba lake na baadae kutupwa jela miezi minane ameachiliwa huru kabla ya kumaliza kifungo chake baada ya kuonyesha tabia nzuri.
Mlowezi Tom Cholmondeley alihukumiwa kwenda jela miezi minane baada ya kesi yake ya mauaji kubadilishwa kuwa kesi ya kuua bila kukusudia.Mlowezi huyo tajiri alimuua kwa kumpiga risasi raia wa Kenya, Robert Njoya aliyeingia kwenye shamba lake lililopo kwenye mkoa wa Rift Valley ili kuwinda wanyama pori.Mlowezi huyo aliachiwa huru ijumaa kabla ya hata ya miezi minane aliyohukumiwa kuisha kwa kile kilichoelezwa kuwa alionyesha tabia nzuri.Wakati alipokuhumiwa kutumikia kifungo cha miezi minane jela mwezi wa tano mwaka huu, mlowezi huyo alikuwa ameishakaa jela miaka mitatu akisubiria hukumu yake.Jaji wa mahakama kuu ya Kenya, Muga Apondi ndiye aliyetoa hukumu hiyo ya miezi minane jela na kusababisha hasira za wananchi mbali mbali wa Kenya waliokuwa wakilalamika kuwa sheria imepindishwa ili kuwabeba matajiri.Jaji Apondi akiielezea hukumu aliyoitoa alisema kuwa mlowezi huyo hakuua kwa kukusudia kwani baada ya kumpiga risasi Robert Njoya, alijaribu kutoa huduma ya kwanza na alimpeleka hospitali.Mwaka mmoja kabla ya kumuua Robert Njoya mlowezi huyo huyo alimuua raia mwingine wa Kenya lakini kesi yake ilifutwa katika hali ya utatanishi.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote