Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, October 22, 2009

Mauaji ya Albino yanaendelea- Mtoto albino auwawa kwa kukatwa shingo

MWANAFUNZI wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Nyawilimilwa, wilayani Geita, Mwanzamwenye ulemavu wa ngozi, Gasper Elikana (10) ameuawa kwa kukatwa shingo na mguu wake kunyofolewa. Mbali na kumuua albino huyo saa 2:30 usiku juzi, wauaji hao walimjeruhi vibaya kwa mapanga, baba yake mzazi, Elikana Ngelela (44). Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi limetangaza zawadi ya sh 1,000,000 kwa yeyote atayetoa taarifa za kukamatwa kwa wahusika, kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Bw. Elias Kalinga alipozungumza na Majira jana jioni baada ya kufika eneo la tukio. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Abbas Kandoro alisema kuwa alipokea taarifa za tukio hilo kwa masikitiko makubwa na kwamba kitendo hicho lazima kikemewa na kila Mtanzania anayejali maisha ya binadamuwenzake. Bw. Kandoro alisema utajiri haupatikani kwa kukata viungo vya albino bali ni watu kufanya kazi kwa bidii ili wajiletee maendeleo. Alisema kuwa serikali inatoa wito kwa jamii kutoa ulinzi kwa walemavu wa ngozi mkoani Mwanza na si kuiachia serikali pekee katika mapambano dhidi ya watu wanaojihusisha na vitendo hivyo vya kinyama. Bw. Kandoro alisema ameagiza timu maalumu kutoka mkoani Mwanza, ikiongozwa na Bw. Kalinga kwenda wilayani Geita kufanya uchunguzi kuungana na Kikosi Kazi kinachoongozwa na Mkuu wa Wilaya yaGeita, Bw. Philemon Shelutete. Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Geita, Dkt.Cassian Kabuche alisema kuwa majeruhi ambaye amelazwa wodi namba nane hospitali hapo hali yake si ya kuridhisha kutokana na majeraha aliyopata kichwani. "Alifikishwa hapa jana (juzi) usiku akiwa hajitambui kiasi kwamba iwapo hali ingeliendelea hivyo hadi leo (jana), tungempeleka katika Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza, lakini kutokana na juhudi zilizozifanya hali yake angalau inatia moyo kidogo," Alisema Dkt.Kabuche.Habari zilizopatikana kijijini hapo, zinasema wauaji hao wakiwa na mapanga, walifika nyumbani kwa Bw. Ngelela na kuanza kumshambulia kwa mapanga na kisha kumuua mwanaye. Mkazi wa kijiji hicho, Bw. Makami Nkilijiwa, alisema majirani walisikia kelele za kuomba msaada kutoka kwa mama wa mtoto huyo, nawalipofika walikuta wauaji wamekwishatoweka na mguu wa kulia wa mtoto huyo, huku mwili wake ukiwa umekatwa shindo huku baba yake akiwa ajitambui. Baada ya kuona hali hiyo, wakazi wa kijiji hicho walimchukua majeruhi na mwili wa marehemu hadi Hospitali ya Wilaya ya Geita ambako maiti imehifadhiwa na majeruhi akiendelea na matibabu.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote