Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, October 27, 2009

Baunsa mdogo kuliko wote duniani huyu hapa

Pamoja na kuwa na umri wa miaka mitano, mtoto Giuliano Stroe ndiye mtoto mwenye nguvu kuliko watoto wote duniani na kutokana na mazoezi makali anayofanya tumbo lake limekatika miraba sita. Mtoto Giuliano Stroe alianza kubeba vyuma, kupiga pushapu na kufanya mazoezi makali tangia alipokuwa na umri wa miaka miwili.Giuliano anaishi na wazazi wake ambao wote ni raia wa Romania katika mji mmoja nchini Italia.Giuliano aliingia kwenye kitabu cha rekodi za dunia mwaka huu baada ya kufanya shoo ya maguvu yake iliyowaacha watu wengi midomo wazi.Shoo hiyo ilirushwa Live na televisheni za nchini Italia.Baba yake Giuliano, Iulian Stroe, 33, alisema kwamba alianza kwenda naye gym tangia alipokuwa mdogo sana. Giuliano alianza kubeba vyuma vya uzito mdogo wakati huo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote