Kesi ya mauji ya kikatili ya watu 17 wa ukoo mmoja imechukua sura mpya baada ya mtu anayesadikiwa kuwa mganga wa kienyeji kuunganishwa kesi ya mauaji inayowakabili watuhumiwa wengine 18. Mganga huyo ambaye ni mwanamke pekee katika kesi hiyo, alitajwa kuwa ni Mariam Sivanus Masatu, anadaiwa kufanikisha mipango ya mauaji hayo. Masatu jana alipandisha kizimbani kwa mara ya kwanza na kusomewa shitaka la kushiriki katika mauaji hayo yaliotokea usiku wa Februari 16, mwaka huu katika eneo la Buhare, nje kidogo ya Manispaa ya Musoma. Mwendesha Mashitaka, Mrakibu wa Polisi, Gabriel Bonanza, alidai mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Husen Mushi, kuwa kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa huyo kunaongeza idadi ya kutoka 19 hadi 20, ingawa alisema mtuhumiwa mmoja kati yao amefariki dunia hivyo kubakia watuhumiwa 19. Alimtaja mtuhumiwa aliyefariki kuwa ni Daudi Nyamagati Makika huku akiitaarifu mahakama kuwa mtuhumiwa mwingine, Bundara Ikaka, alishindwa kufika mahakamani jana kutokana na kuwa mgonjwa na kwamba amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mara. Wathumiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote dhidi ya mashitaka 17 ya mauaji na matatu ya kujaribu kuua ambayo yanawakabili. Walirejeshwa rumande hadi Aprili 14, mwaka huu. Polisi wengi walimwagwa kuimarisha ulinzi ili kuepusha uwezekano wa watuhumiwa hao kushambuliwa na watu wenye hasira. Wakazi wengi wa manispaa ya Musoma walijitokeza kuwashuhudia watuhumiwa wakiingia mahakamani. Hati ya mashitaka iliyosomewa watuhumiwa hao, ilidaiwa kuwa watuhumiwa hao waliwaua watu 17 kwa kukusudia wakati wakijua ni kosa. Watuhumiwa katika kesi hiyo ni Marwa Mau Mgaya (16), Matiko Mgasa, Juma Mgaya, Juma Kinonko, Daudi Nyamagati, ambaye ni marehemu, Aloyce Nyakumu, Bahati Simeo, Nyakangara Wambura na Nyakangara Masemere. Wengine ni Kumbata Alphonce, Alphonce Nyabugimbi, Sodaki Alphonce, Mikindo Mgendi, Mole Magesa, Vedastus Nyangeta na Sospiter Mbita, ambaye ni mwalimu wa Shule ya Nsingi Kukirango Usiku wa Februari 16 mwaka huu katika mtaa wa Bugaranjabho watu wasiofahamika walivamia familia tatu za ukoo mmoja na kuwaua kwa kuwachinja na kuwaatakata mapanga watu 17 wakiwemo watoto wachanga kwa kile kilichadaiwa ni ulipizaji wa visasi.
Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Wednesday, March 31, 2010
Tahadhari kwa wanywaji wa Windhoek na Heineken
KAMPUNI bia ya Mabibo Beer inspirit ya jijini Dar es Salaam imetoa tahadhari kwa wananchi kwa kuwa na wimbi kubwa la uingizwaji wa bia bandia nchini aina ya Heineken na Windhoek. Kampuni hiyo imesema vinywaji hivyo huingizwa nchini kupitia wao lakini kwa sasa kuna watu binafsi wamejitokeza kuingiza bia hizo bandia na kuzisambaza wakitumia nembo hizo kinyume na sheria.
KOVA aamuru kufungwa kwa BAR zote zilizopo karibu na Vituo vya POLICE

`Liyumba ana kesi ya kujibu`

Chanzo: Nipashe
Mama Kikwete anusurika katika ajali Mara

Ujerumani launda Jopo maalum kuchunguza malalamiko ya dhuluma za kijinsia

CCJ yapokea kigogo wa CCM

Monday, March 29, 2010
Mzee wa miaka 96 aoa binti wa miaka 30
kibabu cha umri wa miaka 96 wa nchini Taiwan kimekuwa gumzo nchini humo baada ya kufunga ndoa na mwanamke aliyemzidi miaka 66. Babu Lin Chung ameweka rekodi ya kuwa bwana harusi mwenye umri mkubwa kuliko wote nchini Taiwan baada ya kufunga ndoa na mwanamke mwenye umri wa miaka 30.Chung amekuwa gumzo kwenye kitongoji cha Tainan baada ya kumuoa mwanamke huyo anayetoka maeneo ya ukanda wa kati nchini China katika jimbo la Hunan.Chung ambaye hakuwahi kuoa katika ujana wake, ana watoto wawili aliojitolea kuwalea tangia walipokuwa wadogo ambao hivi sasa mmoja kati ya watoto hao ana umri wa miaka 68.Chung anadai kwamba miaka mitatu iliyopita, alipewa maelezo na Mungu aende kwenye jimbo la Hunan nchini China ili kumtafuta mwanamke anayekuja kuwa mke wake.Chung alifunga ndoa na mwanamke huyo hivi karibuni pamoja na upinzani mkali toka kwa mwanae huyo wa kujitolea ambaye alikuwa akimuona babu huyo kama amelaghaiwa."Inanibidi niwe na mwenza katika uzee wangu... sikuwahi kuwa na mke, kwanini hivi sasa hataki mimi nioe", alisema Mzee Chung.
Balaa lingine Mara!
AJUZA mwenye miaka kati ya 90-100 Sifia Makubo amenyofolewa miguu yake yote miwili kwa panga na sasa yupo hospitali akiwa mahtuti. Ajuza huyo alikumbwa na mkasa huo mwishoni mwa wiki nyumbani kwake Ngerengere kata ya Sirari tarafa ya Inchugu wilayani Tarime Mkoani Mara. Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Tarime /Rorya Costantine Massawe alisema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 27 mwaka huu na ajuza huyo amelazwa katika Hospitali ya Wilaya Tarime. Imedaiwa kwamba ukatili huo amefanyiwa na Mkazi wa kijiji cha Kubiterere ambaye hakufahamika jina lake mara moja. Kamanda Massawe akielezea mkasa huo zaidi alisema mtuhumiwa huyo akiwa na panga alivamia nyumba ya bibi Huyo na kuanza Kumshambulia kwa Kumkata kata mapanga na kumwacha akivuja damu nyingi huku akilia kuomba msaada , Kamanda Massawe alisema kuwa Mjukuu wa Bibi huyo alisikia kilio cha bibi yake kuomba msaada na kuanza kupiga yowe ambapo wananchi Majirani walijitokeza mara moja na kumfukuza hadi walipomtia mikononi na kuanza kumpiga. Mtuhumiwa huyo alikatwa panga tumboni hadi utumbo wote kutoka nje. Polisi Kituo cha Sirari walifika waliwahi kufika kwenye kituo kumuokoa mtuhumiwa kwa kumfikisha hospitalini na ajuza huyo. Mtuhumiwa alifariki siku hiyo hiyo na ajuza huyo bado amelazwa Wodi namba 6 kwa matibabu ya miguu yake yote Miwili na majeraha ya mkono wa kushoto.
Serikali yafikiria kuitanua barabara ya Morogoro?

SERIKALI ipo katika mazungumzo na wahisani ili kuweza kupanua barabara ya Morogoro kuanzia Dar es Salaam hadi Chalinze, kwa kiwango cha njia mbili zitakazosaidia kurahisisha usafiri na kuondokana na ajali zisizo za lazima. Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa alisema hayo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari Ruvu mkoani Pwani, kabla ya Rais Jakaya Kikwete kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa machinjio ya kisasa ya Ruvu iliyopo Ruvu Darajani. Alisema ajali nyingi zinazotokea katika eneo hilo hazitokani na wembamba wa barabara hiyo kama inavyofikiriwa, bali zinatokana na uzembe wa madereva ambapo wengi wao wameonekana wakiendesha kwa kukiuka kanuni za usalama barabarani ikiwemo kwenda mwendo kasi kupita kiasi, kulewa na madereva wengine hupitiwa na usingizi wakiwa waneendesha magari. Dk Kawambwa amezungumza hayo ikiwa ni siku chache baada ya kutokea ajali mbaya katika eneo la Kibamba Darajani jijini Dar es Salaam, ambako watu 10 akiwamo mama mjamzito aliyepasuka tumbo, walifariki dunia papo hapo baada ya lori la mafuta kuiangukia daladala. Wembamba wa eneo ilipotokea ajali ya juzi na kuua watu wote kwenye daladala ni changamoto kwa serikali kutanua barabara hiyo, lakini ajali zinazotokea katika eneo hilo hazitokani na wembbama wa barabara, kwani ajali zinazotokea katika eneo hilo zinatokana na uzembe wa madereva,alisema Dk Kawambwa. Akizungumzia kuhusiana na mradi wa ujenzi wa barabara ya Bagamoyo, Dk Kawambwa alisema mradi huo unatarajiwa kuanza mwaka huu na utaanzia kutanua eneo la Mwenge hadi Tegeta kwa ngazi ya njia mbili za kuingia na kutoka ili kusaidia kuondokana na msongamano wa magari katika barabara hiyo. Tunajua tutapata changamoto kubwa kwa wananchi waliojenga kandokando ya barabara hizo tunazotaka kuzitanua, lakini tutajitahidi kwenda na wakati kwa kuendelea na ujenzi huo huku mazungumzo na wananchi hao katika maeneo mengine ambayo yatakuwa bado hatujayafikia yakiendelea ili kuhakikisha ujenzi huo unafanikiwa kwa kiwango cha njia mbili,alisema Dk Kawambwa. Pia Dk Kawambwa alisema ili kuondokana na tatizo kubwa la msongamano wa magari ndani ya jiji la Dar es Salaam, kupitia mradi wa kutanua barabara 10 za jiji hilo la Dar es Salaam utafanyika kwa lengo la kurahisisha usafiri katikati ya jiji hilo. Alisema mradi huo utafanya kazi kwa kutumia barabara tofauti na zilizo zoeleka katika usafiri wa daladala kama barabara ya Morogoro na Mandela. Tunatarajia kutumia njia nyingine na hazitamlazimisha dereva kutumia barabara moja ya Morogoro ili afike Posta ama Ubungo bali ataweza kupita ya kutokea Kigogo na kumuwezesha kufika ubungo ama Posta hiyo ikiwa ni malengo ya kuondokana na msongamano wa foleni katika barabara hizo. Aliongeza kuwa mradi huo pia utasaidia kuondoa mrundikano wa malori kuwa katika foleni moja na magari madogo hasa katika barabara ya Jangwani, ambapo imeonekana malori yakiitumia pamoja na magari mengine madogo ambapo mradi huo ukianza malori na magari mengine hayatakuwa katika barabara moja.
Mahakama yasomewa waraka kesi ya mauaji
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imepokea waraka ambao inadaiwa uliandikwa na Benson Urio kabla ya kutenda kosa baada ya kushtakiwa kwa jaribio la mauaji. Katika kesi hiyo namba moja ya mwaka 2008, Benson anadaiwa kujaribu kumuua aliyekuwa mpenzi wake, Omega Leweta ambaye ni mkazi wa Kimara jijini Dar es Salaam baada ya kumvizia akiwa usingizini na kuanza kumkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili. Pia mshtakiwa huyo anadaiwa kuwa baada ya kumkatakata mpenzi wake, Benson pia anadaiwa kujikatakata shingoni kwa panga kwa lengo la kujiua sambamba na mpenzi wake huyo. Waraka huo ambao unadaiwa kuandikwa na mshtakiwa huyo kwenda kwa mama yake mzazi, Felister Urio ulisomwa juzi mahakamani hapo na shahidi wa tano katika kesi hiyo D/Sgt. Gotard Ipande wakati akitoa ushahidi katika kesi hiyo. Waraka huo unaonyesha dhamira ya mshtakiwa huyo kumuua mpenzi wake na baadaye kujiua. Katika waraka huo, Benson anaeleza jinsi mama yake alivyomlea na kumtakia maisha mema, lakini baadaye anaanza kueleza jinsi alivyopendana na mpenzi wake hadi wakati anaondoka kwenda Ulaya. Anaeleza jinsi alivyokatisha maisha yake ya barani Ulaya na jinsi ambavyo mpenzi wake hakufurahia kurejea kwake mapema na baadaye kueleza jinsi mpenzi huyo alivyobadilika baada ya kurejea. "Hali niliyokukuta nayo haikuwa nzuri kama nilivyokuzoea. Nilikuuliza una tatizo gani ukajibu hakuna tatizo. Nilikuuliza au umepata mpenzi mwingine ukasema hakuna. Nilivyokufahamu siyo ulivyokuwa na siku zilivyozidi kwenda nilikuuliza kila tulivyozoeana," anasema katika waraka huo. Hadi leo uhusiano wangu kwake hauko, hata ya kusema anachonisemesha ni salamu tu, habari za asubuhi na za saa hizi atokapo kazini. Hata wakati wa kula ni mende tu ndio wanamfukuza chumbani na kumwambia nenda kakae na mwenzako umemwacha; Hata nikimsemesha anaitikia tu sasa jamani naomba kuuliza, ni mapenzi gani haya? Je ni kwa sababu ya kusafiri kwangu? Je, ni kwa sababu ya umaskini wangu jamani kwa vile sina pesa, anahoji. "Uhusiano kwangu si mzuri, isitoshe kashfa na dharau na kejeli zimezidi;Nimegundua Omega ana kiburi kwa sababu ana pesa, siku hizi anajuana na watu wengi, lakini kazi anayofanya katafutiwa na dada yangu Happy lakini leo hata Happy hamthamini." Anaendelea kueleza katika waraka huo kuwa anahisi mpenzi wake alipata bwana wakati akiwa Ulaya na anamshangaa kwa jinsi asivyojielewa kwa kuwa alikuwa mpishi wa chakula, maarufu kama "Mama Ntilie". Anaeleza jinsi alivyomsomesha mwanae Grace tangu darasa la nne hadi sekondari. Anaeleza jinsi alivyotuma dola za Kimarekani 250 na baadaye Sh5.5 milioni kwa ajili ya ubarikio wa Grace na zawadi nyingi zenye thamani ya dola 300 za Kimarekani wakati aliporejea nchini, lakini bado anadharaulika na anamaliza waraka wake kwa kueleza kuwa hana deni bali yeye ndiye anayewadai watu aliowataja na kwamba vitu vyote apewe mama yake.
Chanzo Mwananchi
Friday, March 26, 2010
Mrema adai Sh 1 bilioni kwa Spika Sitta

Spika ni mhimili na kiongozi muhimu katika nchi anatakiwa kuongoza kwa haki tena bila kubagua, lakini yeye anaongoza kwa makundi kwa nini, alihoji. Mrema aliongeza kuwa madaraka aliyoyatumia Sitta yamemvunjia heshima yake aliyokuwa nayo kwa sababu tangu amtolee kashfa hizo baadhi ya wananchi wameanza kumdharau. Watu wote wameshanza kunidharau sasa, hivyi kweli heshima yangu niliojijengea tangu uongozi wangu wote nilipokuwa Serikalini mpaka hapa nilipo leo hii Mwenyekiti wa Chama Taifa halafu natupiwa matusi na kashfa kiasi hicho, mbona amenidhalilisha sana huyu Sitta jamani, alisema Mrema. Mrema aliendelea kuwa, bado anahofia maisha yake kwa kukamatwa na polisi kwa kuwa Sitta yuko katika kamati kuu na ni mjumbe hivyo anaweza kuaminika na mtu yeyote. Aidha Mrema alimtaka Sitta kuacha kutumia jina lake katika kupiga kampeni za kumchafua Rais Kikwete na kuwa kama ana malengo ya kumchafua Rais amfuate moja kwa moja. Hizi ni kampeni chafu, Kama Sitta anataka kumkashfu Kikwete asinitumie mimi apite moja kwa moja akamweleze alisema Mrema. Alisema yeye hawezi kuipigia kampeni CCM kwa kuwa hata yeye ana chama chake na kuwa kama CCM ilipata ushindi wa kishindo katika miaka ya nyuma bila yeye kufanya kampeni iweje iwe mwaka 2010. "Tangu mwaka 1995 hadi 2005 CCM ilipata ushindi wake kwa nguvu bila kupigiwa debe na mrema iweje iwe mwaka huu, mimi ni mtu mdogo sana kwa nafasi hizo" alisema Mrema.
Chanzo: Mwananchi
Vilio, Simanzi vyatanda katika mji mdogo wa Kibamba Dar es salaam
Vilio, simanzi na majonzi, vilitawala jana katika eneo la Kibamba nje kidogo ya katikati ya Jiji la Dar es Salaam, wakati miili ya abiria 11, ukiwamo wa mama mjamzito, ikinasuliwa kutoka kwenye vyuma vya daladala na lori la mafuta ya taa, baada ya magari hayo kugongana uso kwa uso na watu hao kufariki dunia papo hapo. Miili ya watu hao ilinasa katika vyuma hivyo baada ya lori hilo aina ya IVECO lenye namba za usajili T 189 ABP kuligonga daladala hilo aina ya Toyota Hiace lenye namba za usajili T 615 AJW na kisha kulisukuma kwenye mtaro na kulilalia hivyo kufanya kazi ya kuinasua miili hiyo kutoka kwenye vyuma vya magari hayo kuwa ngumu. Daladala hilo linalofanya safari kati ya Mlandizi na Ubungo, lilikuwa likitokea Kibamba wakati lori hilo linalomilikiwa na Mahmoud Mohamed lilikuwa likisafirisha lita 30,000 za mafuta ya taa kutoka Dar es Salaam kwenda Isaka, Shinyanga. Ajali hiyo inayotajwa kuwa moja ya ajali mbaya zilizowahi kutokea jijini Dar es Salaam katika siku za karibuni, ilitokea saa 10:30 alfajiri jana, baada ya lori hilo kutaka kulipita gari lililokuwa mbele yake na kwenda upande wa pili wa barabara ya Morogoro na kuligonga daladala hilo. Kutokana na ajali hiyo, daladala hilo liliharibika vibaya kiasi cha kukutofaa tena kwa matumizi na watu wote 11, wanaume wakiwa wanane na wanawake watatu waliokuwamo walifariki dunia papo hapo na miili yao iliharibika vibaya. Baadhi ya maiti zilishuhudiwa zikiwa zimepasuka vichwa na nyingine viungo vya miili vikiwa vimekatika vipande vipande. Miongoni mwa waliokuwamo kwenye daladala hilo, ni pamoja mama mjamzito, aliyefahamika kwa jina la Zainabu Ally, ambaye pembeni ya mwili wake kulikutwa mkoba uliokuwa na vifaa vinavyotumika wakati wa kujifungua. Haikufahamika mara moja iwapo mama huyo safari yake ya jana kabla ya kukumbwa na umauti, alikuwa akienda hospitali kujifungua au la. Maiti mwingine aliyetambuliwa ni dereva wa daladala hilo, Faraji Ismail Ngalamba, ambaye alikutwa akiwa amenasa kwenye vyuma vya lori hilo. Alinasuliwa baada ya askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji cha Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na wafanyakazi wa Chama cha Msalaba Mwekundu pamoja na polisi kukata vyuma vya lori hilo. Mwingine, ni abiria Shukuru, ambaye alitambuliwa na baba yake mzazi, Hussein Saleh Mwagilo, mkazi wa Kibamba katika eneo la ajali na mwingine alitambuliwa kwa jina la Abutwalib Twaibu. Ajali hiyo ilivutia maelfu ya wakazi wa maeneo ya katikati na nje ya Jiji la Dar es Salaam, ambao walifurika katika eneo la ajali kushuhudia miili ya watu iliyonasa kwenye vyuma vya magari hayo kwa takriban saa 8; kuanzia saa 10:00 alfajiri hadi saa 6:10 mchana. Askari polisi wa kawaida na wale wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), usalama barabarani pamoja na askari kanzu wenye silaha za moto, wakiongozwa na Kamanda wa Kikosi cha Askari wa Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, walifika saa 1:00 asubuhi na kudhibiti eneo lote la ajali. Hatua hiyo ilichukuliwa na polisi, baada ya baadhi ya watu kuvamia eneo hilo muda mfupi baada ya ajali kutokea na kuanza kuiba mafuta kutoka kwenye tanki la lori hilo. Kazi ya kuinasua miili kutoka kwenye vyuma vya magari hayo, ilianza rasmi saa 4:30 asubuhi baada ya gari la kampuni ya Effco Crane la kunyanyua vitu vizito kufika eneo hilo. Kazi hiyo iliyochukua zaidi ya saa mbili; kuanzia saa 4:30 asubuhi hadi saa 6:10 mchana, ilisababisha barabara ya Morogoro kufungwa kwa muda huo. Hata hivyo, awali kazi hiyo ilichelewa kuanza baada ya askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji cha Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, kufika mapema, lakini wakashindwa kufanya lolote kutokana na kuwa na vifaa duni. Hali hiyo ilidhihirika pia, wakati kazi ya kunasua miili hiyo ikifanyika, kwani askari wa kikosi hicho walishuhudiwa wakibeba miili ya watu hao huku wakiwa wamevaa mifuko ya plastiki ya rangi nyeusi badala ya glovu. Maiti mbili; moja ya Shukuru Hussein, nyingine ya mwanamke, ambaye hajatambuliwa pamoja na mguu, baada ya kunasuliwa zilichukuliwa na Land Rover ya polisi na kupelekwa kuhifadhiwa katika Hospitali Teule ya Tumbi, Wilaya ya Kibaha, mkoani Pwani. Maiti nyingine tisa, ambazo hadi tunakwenda mitamboni zilikuwa hazijatambuliwa, zilipelekwa kuhifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), jijini Dar es Salaam. Wakati kazi ya kuinasua miili hiyo ikiendelea, watu waliofika eneo la ajali, walianza kushangilia baada ya mmoja wao aliyejitambulisha kwa jina la Fred Nicodemus, mkazi wa Kibamba, kuangua kilio ghafla katika eneo, ambako lori na daladala hilo zilikuwa zimeanguka. Fred aliangua kilio baada ya kuitambua maiti ya mama yake mzazi, Ester Christiano, aliyekuwa mfanyabiashara wa Kariakoo, jijini Dar es Salaam. Baada ya kusikia sauti ya Fred ikitoka katika eneo yalikokuwa magari hayo, umati wa watu hao walianza kushangilia wakidhani kijana huyo alikuwa miongoni mwa abiria aliyetolewa akiwa hai katika vyuma vya magari hayo baada ya kunusurika katika ajali hiyo. Awali, mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo, Rashid Mfaume, alisema daladala lililopata ajali, lilianza safari Kibaha na inakisiwa walikuwamo abiria kati ya saba hadi 10. Shuhuda mwingine, Frank Msemwa, ambaye ni dereva wa gari la wanafunzi, alisema aliona lori lililosababisha ajali likitaka kulipita gari lililokuwa mbele yake na baada ya dakika chache ikatokea ajali hiyo. Baba mzazi wa marehemu Shukuru, Hussein Saleh Mwagilo, alisema mwanaye mauti yamemfika alipokuwa njiani akienda kuchukua gari kwa tajiri yake kwa ajili ya kufanya kazi. Naye Sajenti Solomon Mwangamilo, ambaye anaishi karibu na eneo ilikotokea ajali hiyo, alisema akiwa nyumbani kwake saa 11:00 alafajiri, alisikia kishindo kikubwa. Alisema aliposikia hivyo, alijua pengine ni ajali ya kawaida, hata hivyo, hakupuuza, bali alivaa sare kisha akatoka na kwenda kwenye eneo la ajali na kuona watu wakiwa wamekandamizwa na magari hayo. Kamanda Mpinga akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la ajali, alisema walifanikiwa kudhibiti eneo la ajali baada ya baadhi ya watu kutaka kuiba mafuta kutoka kwenye tangi la lori lililopata ajali. Alisema lori hilo lilikuwa limebeba lita 30,000 za mafuta ya taa na kwamba kazi ya kunasua maiti za watu waliokufa ilichelewa kuanza kutokana na magari matatu ya kunyanyua vitu vizito yaliyofika mapema kushindwa kufanya kazi hiyo kutokana na kuwa na vifaa duni. “Hii ni changamoto kubwa inayoikabili serikali,” alisema Kamanda Mpinga, ambaye alisema taarifa za awali alizopata zilieleza kuwa waliokufa ni watu wanane.
Vituko Mahakamani
Washtakiwa watatu wanaokabiliwa na kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha, jana walimmwagia kinyesi askari na kutoroka wakati wakiwa kwenye chumba cha mahabusu. Mahabusu hao walikimbia wakiwa uchi huku wakiwa wamejipaka kinyesi mwilini, kabla ya askari kuwakamata na kuwarudisha katika Mhakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam. Washtakiwa hao ambao waliachiwa huru baada ya Hakimu Richard Kabate wa Mahakama hiyo kuwaondolea shitaka hilo, walifikia hatua hiyo baada ya kuwekwa tena chini ya ulinzi na askari kwa ajili ya kurudishwa kituo cha polisi cha Magomeni kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka mengine mapya ya unyang'anyi wa kutumia silaha. Tukio hilo lilitokea mchana wakati askari wakijiandaa kuwatoa washtakiwa chumba cha mahabusu ili wawapandishe kwenye gari wawapeleke kituoni, ndipo washtakiwa walipotoroka wakiwa uchi. Katika sakata hilo, mmoja wa askari ambaye ni askari magereza mwenye namba A 7690 koplo Peter alimwagiwa kinyesi hicho kwenye sare yake na washtakiwa hao. Askari baada ya kuona hali hiyo walifyatua risasi hewani kuwatawanya watu waliokuwepo mahakamani ili wapate nafasi ya kuwafukuza washtakiwa ambao tayari walikuwa wakitokomea mitaani. Hata hivyo askari waliwakamata washtakiwa wawili, ambao walikuwa wakikimbia uchi eneo laKinondoni Bwawani, wakati mshtakiwa mmoja ambaye alikuwa na nguo alikamatwa na wananchi na kupata kipigo kabla ya askari kufika na kumchukua. Washtakiwa hao ambao walikuwa wamechoka kwa kipigo walichukuliwa kwenye gari la polisi lenye namba T213 AMV kupelekwa kituo cha polisi cha Magomeni kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka mapya. Washtakiwa hao waliotoroka ni Rashid Salum, (25), Hamza Abdallh (27) na Juma Mathis (24).
Thursday, March 25, 2010
Mzungu wa Hilton Hotel Dar atupwa selo kwa kumpiga na kumtusi mfanyakazi wake
Kuna Tetesi kuwa General Manager wa Hoteli moja ya Kitalii iliyoko ufukweni ya Hilton the Double Tree ambaye ni Mzungu ameswekwa Rumande kwa kosa la kumpiga mfanyakazi na kumtusi eti sura yake inafanana na Nyani.Taarifa zaidi zimebainisha kuwa mpaka sasa mzungu yuko selo baada ya kukosa mdhamini.
Ajali Mbaya - Kibamba
Kuna habari za kuaminika kuwa kuna Hiace lenye no ya usajili T615 AJW lililokuwa linatokea Ubungo kwenda Mlandizi imegongwa uso kwa uso na Lori la mafuta aina ya Scania lenye no za usajili T192ABP iliyoandika kwa nyuma maandishi yanayosomeka (Yarabi salama)majira ya saa 1 asubuhi ya leo eneo la Kibamba - Morogoro Rd, Dar es Salaam. Ni ajali mbaya na ya kutisha , mmoja wa mashuhuda kashuhudia maiti zisizopungua saba kwenye Hiace na kaongeza kwa kasema kuwa "Scania imeilalia hiace kabisa yaani scania iko juu hiace iko chini hata kuokoa haiwezekani..na sidhani kama kuna mtu atakuwa amepona ila kwenye scania dereva na konda anaweza akawa amepona..sikuwa na kamera ningeweka kupiga picha, Zimamoto wameelekea eneo la tukio . Taarifa zaidi na za kuaminika tutawaletea baadae . Mungu atupe subira na Uvumilivu
Mtoto mwenye jumla ya vidole 31 afanyiwa Operation



23 Wanusurika kwenye ajali ya basi la HEKIMA
WATU 23 wamenusurika kupoteza maisha baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupinduka katika kijiji cha Tanangozi, mkoani Iringa. Ajali hiyo ilitokea jana saa tano asubuhi, baada ya basi la Hekima kulipita gari ndogo lililokuwa limebeba pombe ya kienyeji aina ya ulanzi kisha kuserereka na kupinduka. Basi hilo lililokuwa na abiria zaidi 70 lilikuwa likitoka Mbeya kwenda Dar es Salaam. Akizungunza na vyombo vya habari kwa njia ya simu, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa, Dk George Kabona alisema kati ya majeruhi hao, 13 ni wanaume na kumi ni wanawake na kwamba hali ya majeruhi mmoja ikiwa ni mbaya. "Majira ya saa 6 mchana leo (jana), tulipokea majeruhi 23 kutoka katika ajali ya basi iliyotokea katika kijiji cha Tanangozi. Kati ya hao 13 ni wanaume na kumi ni wanawake na hali zao zinaendelea vizuri, lakini mmoja kati yao hali yake ni mbaya na amelazwa chumba cha wagonjwa mahututi," alisema Dk Kabona. Dk Kabona alisema kuwa kwa mujibu wa majeruhi hao, ajali hiyo ilitokea kutokana na barabara katika eneo hilo kuwa na utelezi uliosababishwa na mvua nyingi zinazoendelea kunyesha mkoani Iringa na mikoa mingine katika Nyanda za Juu Kusini. Alisema kwamba baada ya basi kulipita gari dogo lililokuwa limebeba pombe aina ya ulanzi na dereva kutaka kurudi katika njia yake ndipo liliposerereka na kupinduka. Mmoja wa majeruhi hao alipouliza alisema kuwa ajali hiyo ilitokea baada ya basi (Hekima) kulipita gari dogo lililokuwa limebeba pombe ya ulanzi na kuserereka kutokana na barabara kuwa na utelezi uliosababishwa na mvua," alibinisha Dk Kabona.
Mvua Kubwa yatishia Mwanza
MVUA kubwa iliyonyesha jana alfajiri jijini hapa kwa saa mbili imezikosesha makazi zaidi ya kaya 24 za mtaa wa Mabatini Kusini na 10 za Mabatini Kaskazini. wakazi wa kaya hizo walionekana katika harakati za kukusanya vyombo na mali zao zingine zikiwa zimelowa maji na baadhi ya nyumba zikiwa zimebomoka. Akizungumza katika mtaa wa Mabatini Kusini, Mwenyekiti wa Mtaa huo, Yohana Nono, alisema msaada wa haraka wa mahema, vyakula na nguo unahitajika kuwasitiri baadhi ya wananchi ambao vitu vyao vilisombwa na mafuriko ya maji. “Baada ya kufanya tathmini na wananchi wa mtaa wangu, tumebaini kuna jumla ya watu 100 wa kaya 24 ambao nyumba zao zimebomolewa na mafuriko, “ alisema Nono na kuongeza kuwa wanafanya juhudi ya kuwasiliana na uongozi wa wilaya ili kuona uwezekano wa kuwasaidia wananchi hao. Kati ya watu walioathiriwa na mafuriko hayo ni pamoja na Stella Robert (6), ambaye kwa mujibu wa mjumbe wa nyumba 10 shina la Mabatini Kusini mtaa wa Benjamin, Anthony Msafiri, alishtuka saa 10.45 alfajiri na kusikia kelele za watu wakiomba msaada. “Kwanza nilifikiri tumevamiwa na majambazi, maana nilikuwa usingizini, lakini baada ya kuamka nilishuhudia nyumba zote zimejaa maji huku vitu vikielea, nilimkuta Mama Nyanjige - mama mzazi wa Stella aliyesombwa maji, akilia akiniomba kumwokoa Stella,” alisema Msafiri. “Nilichukua tochi na kufuatilia mkondo wa maji, nikawatoa baadhi ya watoto walionasa kwenye baadhi ya nyumba na kuelekea kambi ya Polisi Mabatini, ambako tulikutana na maaskari na tulipowauliza, wakasema Stella aliokolewa na mwanamke. “Alikuwa akielea huku akipiga kelele za kuomba msaada kwa maaskari hao, ndipo walipochungulia dirishani wakamwona na kuokolewa na mke wa askari,” alisema na kuongeza kuwa walimpeleka kituo cha afya na hatimaye hospitali ya mkoa ya Sekou Toure alikolazwa. Wakizungumza kwa uchungu mbele ya wananchi waliofurika eneo hilo, waathirika Issa Mauba, Tatu Ally na Hassan Babu, walidai kuwa chanzo cha mafuriko ya mara kwa mara Mabatini ni ujenzi usiozingatia mipango. Hii ni mara ya pili katika kipindi kifupi, Jiji la Mwanza kukumbwa na mafuriko huku ya hivi karibuni yakisababisha watu sita kupoteza maisha na zaidi ya 200 makazi. Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Wilson Kabwe, alisema tayari timu ya wataalamu imefika mitaa hiyo ya mafuriko ingawa hakukuwa na athari za kutisha. “Timu yangu ya wataalamu imefika maeneo yaliyopata mafuriko na tutatoa taarifa baadaye na tuone nini cha kufanya juu ya waathiriwa wa mafuriko, baada ya mvua ya jana,” alisema Kabwe.
Mwanamke aenda jela Miaka 7 kwa kufanya mapenzi na mtoto wa Miaka 15 Moshi
MWANAMKE ambaye ni mke wa mtu mwenye watoto watatu, amehukumiwa kifungo cha miaka saba jela baada ya kupatikana na hatia ya kufanya mapenzi na mwanafunzi wa kidato cha kwanza mwenye umri wa miaka 15. Mwanamke huyo, Sophia Philemon (44) mkazi wa kambi namba tisa katika kiwanda cha sukari cha TPC, wilaya ya Moshi vijijini kuhukumiwa kifungo hicho, pia ameamriwa kumlipa mwanafunzi huyo fidia ya Sh1 milioni. Hukumu hiyo, ilitolewa jana mjini Moshi na Kaimu Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa Kilimanjaro, John Nkwabi baada ya kuridhika na ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa mashitaka. Nkwabi alisema ushahidi wa mashahidi hao, akiwemo mwanafunzi huyo wa sekondari ya Langasani, umeithibitishia mahakama kwamba mwanamke huyo, alimlazimisha mtoto huyo kufanya naye tendo la ndoa. Kitendo hicho ni kosa chini ya kifungu namba 138B (1) (d) cha kanuni ya adhabu kinachosimamia makosa ya kimapenzi kwa watoto baada ya sheria hiyo kufanyiwa marekebisho mwaka 2002. Hakimu Nkwabi alisema mahakama imeridhika na ushahidi kuwa Februari 28, mwaka jana, saa 1:00 usiku huko kambi namba tisa, mshitakiwa alimlazimisha mwanafunzi huyo kufanya naye mapenzi katika chumba anachoishi na mumewe. Muda huo, mwanafunzi huyo alikuwa ametoka dukani alikokuwa ametumwa na wazazi wake na mwanamke huyo, alimwita na kumshawishi aingie ndani ya nyumba yake na baadaye kumlazimisha kufanya naye tendo la ndoa. Baada ya kutiwa hatiani, wakili wa serikali, Hellen Moshi aliyeendesha kesi hiyo, aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwani vitendo vya ubakaji vinazidi kuongezeka nchini hususani kwa watoto wadogo na wanafunzi. Katika utetezi wake, Sophia alisema ni mke wa mtu na hakubahatika kupata mtoto na mwanaume huyo, lakini kabla kuolewa alikuwa tayari amezaa watoto watatu, wawili wa kike na mmoja wa kiume. Mshitakiwa alikataa kufanya tendo la ndoa na mtoto huyo, licha ya kumfahamu kuwa ni jirani yake. Utetezi wake ulitupiliwa mbali na mahakama hiyo.
Mshindi wa Miss Universe 2009 alamba BINGO

Wednesday, March 24, 2010
Mapenzi yampeleka Kaburini yeye na mtoto wake
Katika hali ya kusikitisha, mwanaume aliyetambuliwa kuwa ni Mwidadi Hamisi,(32) mkazi wa Bombambili mjini Songea, mkoani Ruvuma, amemnyonga mtoto wake wa umri wa miaka minne na baadaye naye kujinyonga huku akiwa ameacha ujumbe kuwa uamuzi huo umetikana na shida alizokuwa akipata kutoka kwa mke wake wa zamani.Tukio hilo lilisikitisha wengi hasa kwa kitendo cha kumnyonga mtoto Mulla, ambaye hakuwa na hatia, lilitokea saa 5:00 asubuhi wiki iliyopita katika maeneo ya Mlima wa Chandamali,nje kidogo wa mji wa Songea.Kabla ya kuamua kujinyonga, marehemu ambaye wakati wa uhai wake alikuwa mwendesha pikipiki zinazosafirisha watu,alimpiga simu kwa tajiri wake akimtaka afuate pikipiki yake katika maeneo ya mlimani huo.Habari zilisema katika simu hiyo marehemu alimwambia tajiri yake kuwa yeye ameamua kwenda kupumzika kaburini na mtoto wake, ili kuepuka shida alizokuwa akizipata kutoka kwa mke wake wa zamani.Kabla ya kujinyonga, Mwadadi, aliacha ujumbe huku akiambatanisha na orodha ya namba za simu za ndugu zake na kutaja sehemu anakotoka kuwa Newala mjini mkoani Mtwara.Katika ujumbe huo, marehemu alisema ameamua kujinyonga yeye na mtoto wake kufuatia kashfa alizokuwa akizipata kutoka kwa mama watoto wake.Katika ujumbe huyo marehemu alimtuhumu mama huyo kuwa amekuwa akimweleza mpenzi wake, siri za maungoni mwake.Akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio tajiri wa marehemu huyo,Hussein Msafiri, alisema siku kadhaa zilizopita, marehemu aliwahi kumweleza matatizo yake yeye na mke wa zamani."Mara nyingi alionekana mtu ambaye hana amani moyoni mwake," alisema
Nafasi ya Kazi
The EC Delegation in Tanzania wanahitaji mfanyakazi wa muda kwa nafasi ya Receptionist / Telephone Operator, ili kuziba nafasi ya mtu anayeenda kwenye Likizo ya Uzazi kuanzia 15 April hadi 30 July 2010. Maombi yote yatumwe kwa :Ms May Kazuka Admin Assistant / Personnel EC Delegation Tanzania Umoja House, Garden Avenue Dar es Salaam Simu: +255 22 2117473-6 Fax:+255 22 2113277 Email: May.KAZUKA@ec.europa.eu
Tuesday, March 23, 2010
Wanafunzi IFM wagoma kupinga ongezeko la ada
WANAFUNZI wa Shahada ya kwanza na ya pili katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha [IFM] jana waligoma kuendelea na masomo kutokana na ongezeko la ada lililopanda ghafla. Wanafunzi hao jana waliamua kuweka mgomo baada kupinga ongezeko la ada zaidi ya asilimia 50% .Walionekana kuandamana kwenda kutaka kumuona mfadhili wa chuo hicho ambae ni Waziri wa Fedha ili wamueleze tatizo hilo kama ana taarifa nalo.Wanafunzi hao waliweka mgomo huo baada ya kutopata majibu ya matokeo ya mitihani baada ya kuambiwa hadi wamalize ada na kushangazwa na kauli hiyo.Wanafunzi hao walidai kuwa ada zimepanda kutoka shilingi milioni moja hadi kufika milioni moja na laki sita jambo ambalo limewashangaza kupanda kwa ada hizo bila ya kupewa taarifa rasmi.
Gari inauzwa (Pichani)
Kashfa Kubwa yaikumba Afrika ya Kusini - Yamfunga Mwanamke Jela ya Wanaume Kwa Miezi Sita
Skendo limeikumba kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini ambapo mwanamke aliyakamatwa kwa makosa ya ujambazi anadaiwa kufungwa kwenye jela ya wanaume kwa kipindi cha miezi sita na kupelekea mwanamke huyo abakwe na kulawitiwa na wafungwa wa kiume.Denise Wilson au maarufu kwa jina la Abbah wa mji wa Isipingo nchini Afrika Kusini amekifungulia mashtaka kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini kwa kumweka kwenye jela ya wanaume kwa miezi sita wakati alipokuwa akisubiria kufikishwa mahakamani kwa makosa ya ujambazi, kujaribu kuua na kuteka watu.Denise anadai fidia ya rand 100,000 kwa madhila aliyoyapata wakati alipokuwa kwenye jela ya wanaume.Katika nyaraka za mahakama, Denise alisema kuwa alikamatwa septemba 24 mwaka 2002 na kupelekwa kwenye jela ya wanaume.Alisema kuwa kitendo chake cha kupinga kuwekwa jela moja na wanaume kilisababisha avuliwe nguo mbele ya wanaume huku akizomewa na kuchekwa.Wakati wa kipindi chake cha miezi sita kwenye jela ya wanaume, Denise anadai kuwa walinzi wa jela walikuwa wakimlazimisha afanye matendo ya ngono bila ya idhini yake.Alidai pia kuwa wafungwa wa kiume walikuwa wakimpapasa mara kwa mara kwenye sehemu zake za siri bila ya idhini yake.Denise pia hakusita kusema kuwa alibakwa na kulawitiwa katika kipindi cha miezi sita kwenye jela ya wanaume.Alisema kuwa ingawa maafisa wa jela walikuwa wakijua kuwa yeye ni mwanamke, waliendelea kumweka jela moja pamoja na wanaume.Alisema kuwa hata daktari wa wilaya alipomfanyia uchunguzi wa kuthibitisha jinsia yake, aliendelea kuwekwa kwenye jela hiyo.Kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini kimeamua kukaa kimya kikisubiria kesi hiyo ianze kusikilizwa mahakamani.
Hatima ya LIYUMBA Ni April 9 ,Mahakama yaombwa kutupilia mbali kesi inayomkabili

Chanzo : Mwananchi
Kwa issue hii lazima wanawake waheshimike
Acheni niwape heshima iliyotukuka wanawake woote duniani
Mmmm jaribu kufikiri haya
Mmmm jaribu kufikiri haya
ANAKUFUMANIA: Analia, ananyamaza, anasononeka, unambembeleza anakuelewa anakusamehe halafu anasahau!!!
UNAZAA NJE YA NDOA: Anasononeka na kulia sana . Anakuchukia lakini baadaye anakusamehe. Halafu analea mtoto uliyemzaa nje kwa upendo. Kama ni kuchukiwa atachukiwa mtoto, si wewe uliyefanya umalaya!
UNARUDI USIKU WA MANANE UKIWA MTUNGI: Anakukaribisha, anakuandalia chakula, unagoma kula. Anahifadhi chakula alichokuandalia bila manung'uniko.
UNAAMKA ASUBUHI NA MAHANGOVER: Anakuandalia staftahi (saa nyingine unagoma kutumia staftahi yake unakimbilia baa kwenda kunywa Supu na kuzimua. Wala halalamiki!CHAKULA CHA USIKU: Ushapiga mtungi wako, unataka huduma. Unamrukia, hamna maandalizi unamuumiza. Anavumilia ili akuridhishe. Na kesho yake tena inaweza tokea hii; hana kinyongo!
UNAJIANDAA KWENDA KIBARUANI: Unakuta kashakuandalia viwalo, suruali imenyooshwa kama ya askari trafiki, shati limepigwa pasi ya maana! Nguo ulizovua jana zimeshalowekwa tayari kwa kufanyiwa usafi! Ulichomuudhi jana kashasahau na kukusamehe!
UNAMPA UJAUZITO: Anauthamini, anautunza anajifungua kwa uchungu, mtoto anakuachia wewe umpe jina, la kwake halimo kabisa kwenye majina atakayotumia mtoto! Na pamoja na uchungu wa kuzaa, bado yuko radhi kukuzalia mtoto mwingine na mwingine tena!Na mengine meeeeengi sana wanafanyiwa hawa watu lakini WANASAMEHE, WANAVUMILIA! Ni watu muhimu sana hawa watu maishani mwangu! HIVI INGEKUWA WANAUME
WANAFANYIWA HIVI INGEKUWAJE?
WANAFANYIWA HIVI INGEKUWAJE?
Monday, March 22, 2010
Namibia wamkumbuka Nyerere

Thursday, March 18, 2010
Wednesday, March 17, 2010
Mchungaji adaiwa kuua mwanaye kwa kumuibia Sh. 50,000
Mchungaji wa Kanisa la African Inland Church (AIC), Jonathan Sabuni (60), Mkazi wa kijiji cha Kasamwa wilayani Geita, Mkoa wa Mwanza, ameua mwanaye Amos Jonathan (16), kwa kipigo kwa tuhuma za kumwibia Sh. 50,000. Marehemu Amos alikuwa anasoma darasa la saba katika Shule ya Msngi Nyampa. Inadaiwa kuwa siku mbili kabla ya kutenda ukatili huo, mtuhumiwa aliikusanya familia yake ya watu wanne na kuwataka waombe baada ya kupotea kwa fedha hizo alizokuwa amepanga kuzifanyia ukarabati wa nyumba ya familia. Mbali na marehemu, wanafamilia wengine ni Baraka Jonatan (18) anayesoma kidato cha pili na mkewe, Esther Jonatahan. Inadaiwa kuwa mchungaji huyo mkewe na kuwataka waombe kuhususiana na upotevu wa fedha hiyo iliyokuwa kwa ajili ya ukarabati wa nyumba ya familia. Imedaiwa kuwa Machi 13, siku mbili baada ya mtuhumiwa kutoa muda kwa marerehemu kurejesha fedha hiyo na kufanya Ibada maalum aliyowakutanisha wanafamilia baada ya marehemu kukiri kuwa ndiye aliyeiba fedha hizo na kuahidi kuzirejesha lakini hakufanya hivyo. Akizungumzia tukio hilo, Esther Jonathan, mama mzazi wa marehemu Amos alisema jana kuwa siku iliyofuata marehemu kwa woga aliamka alfajiri na kuondoka nyumbani kukwepa hasira ya baba yake lakini ilipofika saa nne alimtuma kaka yake Baraka kumrejesha nyumbani. Alisema wakiwa nyumbani saa tano ndipo mtuhumiwa alipoanza kumpiga marehemu kwa fimbo, rungu na mateke akidai marehemu alikuwa ameficha fedha hizo. Mama huyo alisema kuwa alijaribu kuingilia kati kumzuia mumewe kumpiga marehemu, lakini hakumsikiliza. Alisema ilipofika saa moja jioni marehemu alionekana kuzidiwa na ndipo mtuhumiwa alipoacha kumpiga na kwamba hali ya marehemu ilizorota ghafla na ilipofika saa 4:45 usiku mtuhuiwa alimwita Mchungaji Charles Mpanduji wa AIC kumuombea. Hata hivyo, kabla ya kumwita mchungaji mwenzake kumuombea marehemu, mtuhumiwa alimwosha marehemu mwili wote kumuondoalea uchafu kabla ya kukata roho. Kwa mujibu wa Ester, baada ya kugundua kuwa marehemu amekata roho, ndipo mtuhumiwa alipotoka nje na kisha kumuaga mkewe kuwa alikuwa anatoka kuelekea kusikojulikana, lakini yeye Ester) alimshtukia na kumzuia Kwa kumkaba shati asiondoke huku akipiga kelele kutaka msaada wa majirani, lakini baadaye alizidiwa nguvu na kumponyoka na ndipo mtuhumiwa alipotoroka. Kamanda wa Polsisi wa Mkoa wa Mwanza, Simon Sirro, alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo.
Tuesday, March 16, 2010
Trawu, wafanyakazi TRL kutoa tamko leo
CHAMA cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu) kitakutana na wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) ili kutoa tamko la pamoja baada ya serikali kutangaza azma ya kuchukua hisa za mwekezaji ambaye ni Rites ya India. Tamko hilo linakuja wakati zikiwa zimepita siku chache tangu serikali kutangaza azma hiyo ya kuchukua hisa zake ambazo ni asilimia 51 kutoka Rites ambayo ilitakiwa iwekeze dola 8 milioni za Kimarekani (sawa na zaidi ya Sh10 bilioni za Kitanzania) katika mkataba wake wa miaka 25 ulioanzia mwaka 2007. Katibu mkuu wa Trawu, Sylvester Rwegasira aliiambia Mwananchi jana kuwa hatua hiyo itaweka sawa suala hilo kutokana na wafanyakazi kuwa na mawazo tofauti tangu serikali itangaze azma hiyo. Kesho tutakutana na wafanyakazi ili kupata tamko la pamoja ambalo litakuwa limebeba mawazo na maoni ya wafanyakazi wote wa TRL hasa baada ya serikali kuamua kununua hisa, alisema Rwegazira. Kama kutakuwa na mabadiliko yeyote ya muda au chochote, tutafahamishana lakini ni lazima tukutane na kutoa tamko la pamoja. Tangu serikali itangaze azma yake, wafanyakazi wa TRL waliokuwa wakizungumza na vyombo vya habari walikuwa wakitoa maoni tofauti, hali ambayo Rwegasira alisema inatakiwa imalizwe kwa wafanyakazi wote kukutana. Ili serikali iachane na Rites haina budi kutoa taarifa ya miezi mitatu kwa kampuni hiyo inayomilikiwa na serikali ya India na itatakiwa imlipe mwekezaji huyo Sh54 bilioni kama fidia za gharama mbalimbali na matumizi ambayo kampuni hiyo iliingia wakati wa kipindi cha uwekezaji na fedha nyingine Sh56 milioni ambazo zinatakiwa zilipwe kwa kampuni binafsi ya ulinzi ya Ultimate Security. Rites imekuwa ikidai kuwa haistahili kubebeshwa lawama kutokana na TRL kushindwa kuendeshwa kwa ufanisi kwa kuwa serikali ndiyo iliyoshindwa kutekeleza wajibu wake kwenye mkataba. Mkurugenzi mtendaji wa TRL, Hundi Chaundhary aliwaambia waandishi wa habari mwaka jana kuwa serikali inashindwa kuwaeleza wananchi yaliyomo kwenye mkataba ndio maana kampuni hiyo kubwa ya uendeshaji wa huduma za reli inalaumiwa.
Chanzo: Mwananchi
Hatima ya Liyumba kujulikana April 9
Aona kwa kutumia ulimi


Maiti ya Dereva Taxi yakutwa na Tundu
UTATA umezidi kuzingira kifo cha dereva teksi anayedaiwa kuuawa kwa kupigwa na polisi wa kituo cha Chang'ombe jijini Dar es Salaam, baada ya familia kudai kuwa maiti ya kijana wao imekutwa ikiwa na tundu na uvimbe kichwani. Familia hiyo pia imesema maiti ya kijana wao, Mussa Juma, 27, pia imekutwa ikiwa imebabuka sehemu za siri, jambo ambalo linawatia mashaka ndugu. Familia ilitoa madai hayo mara baada ya kuuchukua mwili wa dereva huyo kutokana na madaktari kumaliza uchunguzi wao wa kutaka kubaini sababu ya kifo cha kijana huyo ambaye polisi imedai kuwa alifariki wakati akipelekwa Hospitali ya Temeke baada ya kulalamika hajisikii vizuri wakati akihojiwa. Akizungumza na gazeti hili jana Mwijuma Mzee, ambaye pia ni mjomba wake marehemu Mussa, alisema: Mimi kama mwanafamilia ninachoweza kukueleza ni kwamba mwili huo umekutwa na tundu sehemu ya mguu wa kushoto... sielewi limetokana na nini; uvimbe kichwani na amebabuka sehemu za siri. Hiki ndicho nilichoshuhudia na ninachoweza kukueleza." Mzee alibainisha kuwa kutokana na hali hiyo familia hiyo ina hofu kuwa ndugu yao aliteswa kabla ya kufikwa na mauti, lakini akasisitiza kuwa majibu ya awali yatakayotolewa na daktari aliyefanyia uchunguzi maiti hiyo, yatasaidia kupata ukweli wa tukio hilo. Alisema wanatarajia kupata majibu hayo ya daktari leo na kwamba vipimo zaidi vimepelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali kwa ajili ya utambuzi zaidi. Alisema sababu za kitaalamu za kupeleka vipimo hivyo kwa mkemia mkuu ni baada ya mwili huo kukutwa umejaa hewa na uvimbe, jambo alilosema linasababisha utata katika kupata ukweli halisi wa kifo chake. Tumeambiwa na mganga wetu kuwa vipimo zaidi vya mwili wa marehemu vinatarajia kupelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali ambaye atatoa majibu ya mwisho ya ukweli wa kifo hicho,alisema Mzee. Akizungumzia taratibu za msiba huo, Mzee alisema familia hiyo leo inatarajia kuupokea mwili huo rasmi na kuusafirisha hadi Bagamoyo mkoani Pwani kwa maziko. Alisema msafara huo utaanza majira ya saa 4:00 asubuhi ukitokea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako maiti hiyo imehifadhiwa baada ya kuhamishwa kutoka Hosptali ya Manispaa ya Temeke. Kabla ya kufanyika kwa uchunguzi wa mwili huo familia hiyo ilikataa mwili huo kuchunguzwa ukiwa Hospitali ya Temeke ukidai kuwa wataalamu wa suala hilo wanapatikana Muhimbili na pia kuhofia polisi wa Chang'ombe kuingilia kazi hiyo. Kauli hiyo ya ndugu wa marehemu imekuja siku moja kabla ya mganga aliyefanya kazi ya kuupima mwili wa marehemu hajatoa majibu yake. Sakata la kifo cha dereva huyo liliibuliwa na wanafamilia Machi 10 baada ya kufuatilia kukamatwa kwake kwenye kituo hicho cha polisi na kueleza kuwa amefariki dunia. Inadaiwa kuwa dereva huyo aliuawa na askari hao wakati wakimuhoji kuhusu tukio la ujambazi lililotokea hivi karibuni. Familia inadai kuwa kijana huyo alikamatwa Machi 8 saa 3:00 usiku eneo la Mivinjeni wakati akielekea nyumbani kwake Mtoni Mtongani baada ya muda wa kazi kumalizika. Familia pia inadai kuwa kijana huyo aliuawa siku aliyokamatwa, yaani Machi 8, lakini kamanda wa polisi wa kanda ya Dar es salaam, Suleiman Kova alisema kijana huyo alifariki Machi 10 wakati akikimbizwa hospitalini.
Chanzo: Mwananchi
Ali Ameir kung`atuka ubunge

Chanzo: Nipashe
MV Serengeti yateketea kwa Moto
Meli ya MV Serengeti imeteketea kwa moto siku ya jumapili na mabaharia wanane wamenusurika kufa, wakati ikiwa imetia nanga nje ya bandari ya Malindi mjini Zanzibar. Moto huo ulianza kuwaka majira ya saa 6:30 mchana na kusababisha wasiwasi mkubwa katika eneo hilo lenye ukanda wa hoteli nyingi za kitalii, baada ya umati wa watu kuvamia maeneo hayo wakitaka kushuhudia moto huo. Mrajisi wa Meli Zanzibar, Abdallah Mohammed, alisema kwamba moto huo hadi juzi mchana ulikuwa unaendelea kuzimwa kwa kutumia Tagi ya Shirika la Bandari Zanzibar (ZPC), pamoja na vifaa vya uokoaji kwenye majanga ya moto vilivyomo ndani ya meli hiyo. Hata hivyo, alisema ni mapema kueleza mabaharia wangapi walikuwemo ndani ya meli hiyo na chanzo cha moto huo, hadi hapo uchunguzi wa kitaalam utakapofanyika. Mohamed alisema meli hiyo inamilikiwa na kampuni ya JAK Enterprises L.T.D iliyosajiliwa Zanzibar na kwamba kwa mara ya mwisho ilifanyiwa ukaguzi kati ya Januari na Desemba mwaka jana. “Ukaguzi wa mwisho ulionyesha meli ni nzima na ndiyo maana ikaruhusiwa kutoa huduma ya kubeba abiria na mizigo” alisema Mrajisi huyo wa meli. Alieleza kwamba leseni ya meli hiyo inaruhusu kubeba abiria 550 na tani 100 za mizigo na ilikuwa ifanye safari jana usiku kuelekea kisiwani Pemba. Alisema hilo ni tukio la pili la meli za abiria kuungua moto zikiwa zimeshusha nanga nje ya bandari ya Malindi, ambapo hivi karibuni meli za MV Aziza I na Aziza II ziliteketea kwa moto wakati zikifanyiwa matengenezo katika eneo la Mtoni, nje kidogo ya Bandari ya Malindi. Hata hivyo, alisema kwa mujibu wa sheria abiria wote waliokuwa wasafiri na meli hiyo jana usiku wanapaswa kurejeshewa fedha zao au watafutiwe usafiri mwingine wa kuwafikisha. Kwa upande wake, Mkuu wa Operesheni wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar, alisema ni mapema kuelezea chanzo cha moto huo na mabaharia waliokuwemo hadi hapo kazi ya uokoaji itakapokamilika. “Ni mapema kusema chanzo cha moto isipokuwa hatua za uokoaji zinaendelea na sehemu kubwa ya moto imekwisha dhibitiwa”, alisema Mkuu huyo wa Opereshen.
Mtu Mfupi kuliko wote Duniani afariki

KenolKobil kununua mali za BP Tanzania
.jpg)
Chanzo: Nipashe
Monday, March 15, 2010
Pengo azindua hospitali Kibangu

Subscribe to:
Posts (Atom)
VJN Super Motors
Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote