Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 16, 2010

Maiti ya Dereva Taxi yakutwa na Tundu

UTATA umezidi kuzingira kifo cha dereva teksi anayedaiwa kuuawa kwa kupigwa na polisi wa kituo cha Chang'ombe jijini Dar es Salaam, baada ya familia kudai kuwa maiti ya kijana wao imekutwa ikiwa na tundu na uvimbe kichwani. Familia hiyo pia imesema maiti ya kijana wao, Mussa Juma, 27, pia imekutwa ikiwa imebabuka sehemu za siri, jambo ambalo linawatia mashaka ndugu. Familia ilitoa madai hayo mara baada ya kuuchukua mwili wa dereva huyo kutokana na madaktari kumaliza uchunguzi wao wa kutaka kubaini sababu ya kifo cha kijana huyo ambaye polisi imedai kuwa alifariki wakati akipelekwa Hospitali ya Temeke baada ya kulalamika hajisikii vizuri wakati akihojiwa. Akizungumza na gazeti hili jana Mwijuma Mzee, ambaye pia ni mjomba wake marehemu Mussa, alisema: Mimi kama mwanafamilia ninachoweza kukueleza ni kwamba mwili huo umekutwa na tundu sehemu ya mguu wa kushoto... sielewi limetokana na nini; uvimbe kichwani na amebabuka sehemu za siri. Hiki ndicho nilichoshuhudia na ninachoweza kukueleza." Mzee alibainisha kuwa kutokana na hali hiyo familia hiyo ina hofu kuwa ndugu yao aliteswa kabla ya kufikwa na mauti, lakini akasisitiza kuwa majibu ya awali yatakayotolewa na daktari aliyefanyia uchunguzi maiti hiyo, yatasaidia kupata ukweli wa tukio hilo. Alisema wanatarajia kupata majibu hayo ya daktari leo na kwamba vipimo zaidi vimepelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali kwa ajili ya utambuzi zaidi. Alisema sababu za kitaalamu za kupeleka vipimo hivyo kwa mkemia mkuu ni baada ya mwili huo kukutwa umejaa hewa na uvimbe, jambo alilosema linasababisha utata katika kupata ukweli halisi wa kifo chake. Tumeambiwa na mganga wetu kuwa vipimo zaidi vya mwili wa marehemu vinatarajia kupelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali ambaye atatoa majibu ya mwisho ya ukweli wa kifo hicho,alisema Mzee. Akizungumzia taratibu za msiba huo, Mzee alisema familia hiyo leo inatarajia kuupokea mwili huo rasmi na kuusafirisha hadi Bagamoyo mkoani Pwani kwa maziko. Alisema msafara huo utaanza majira ya saa 4:00 asubuhi ukitokea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako maiti hiyo imehifadhiwa baada ya kuhamishwa kutoka Hosptali ya Manispaa ya Temeke. Kabla ya kufanyika kwa uchunguzi wa mwili huo familia hiyo ilikataa mwili huo kuchunguzwa ukiwa Hospitali ya Temeke ukidai kuwa wataalamu wa suala hilo wanapatikana Muhimbili na pia kuhofia polisi wa Chang'ombe kuingilia kazi hiyo. Kauli hiyo ya ndugu wa marehemu imekuja siku moja kabla ya mganga aliyefanya kazi ya kuupima mwili wa marehemu hajatoa majibu yake. Sakata la kifo cha dereva huyo liliibuliwa na wanafamilia Machi 10 baada ya kufuatilia kukamatwa kwake kwenye kituo hicho cha polisi na kueleza kuwa amefariki dunia. Inadaiwa kuwa dereva huyo aliuawa na askari hao wakati wakimuhoji kuhusu tukio la ujambazi lililotokea hivi karibuni. Familia inadai kuwa kijana huyo alikamatwa Machi 8 saa 3:00 usiku eneo la Mivinjeni wakati akielekea nyumbani kwake Mtoni Mtongani baada ya muda wa kazi kumalizika. Familia pia inadai kuwa kijana huyo aliuawa siku aliyokamatwa, yaani Machi 8, lakini kamanda wa polisi wa kanda ya Dar es salaam, Suleiman Kova alisema kijana huyo alifariki Machi 10 wakati akikimbizwa hospitalini.
Chanzo: Mwananchi

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote