Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, March 8, 2010

Wanafunzi wawili wafa maji wakiogelea

WANAFUNZI wawili wa Shule ya Msingi Makabe, Livingston Richard (10)na mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Abdala (11), wamefariki dunia baada ya kuzidiwa na maji wakati wakiogelea. Watoto hao ambao walikuwa wakiongelea na wenzao katika Bwawa la Asili la linalojulikana kwa jina Rwegasira lilipo Mbezi Makabe jijini Dar es Salaam walifariki dunia baada ya kuzidiwa na maji. Kamanda wa polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga alisema tukio hilo, lilitokea juzi saa 11:30 jioni Makabe kwenye Bwawa la Asili linalojulikana kwa jina la Rwegasila. Kalinga alisema miili ya watoto hao, iliopolewa na wananchi wa eneo hilo, na maiti za watoto hao, zimehifadhiwa katika hospitali ya Tumbi iliyopo Kibaha na upelelezi wa dhidi ya vifo hivyo unaendelea. Katika tukio lingine, Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Ari iliyopo Tabata, Abdallah Miti (18), amefikishwa mahakamani kujibu tuhuma za wizi wa Sh 5 milioni mali ya Anselem Sigela.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote