Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, March 8, 2010

Maalim Seif augua ghafla na kulazwa akisubiri ndege kwenda Oman

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad (pichani), ameugua ghafla wakati akijiandaa kupanda ndege kwenda Muscat, Oman. Baada ya kukatisha safari hiyo, Maalim Seif alipelekwa na kulazwa katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam ambako alikuwa akiendelea kupata matibabu hadi jana jioni. Afya ya Maalim Seif ilianza kuzorota ghafla muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akitokea Zanzibar Ijumaa kwa ajili ya kupanda ndege. Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Chama hicho, Ismail Jussa Ladhu, alithibitisha kuugua kwa kiongozi huyo. Ladhu ambaye ni Mbunge wa Kuteuliwa na mshauri wa Maalim Seif wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, alisema kuwa kiongozi huyo alilazimika kupelekwa katika Hospitali ya Hindu Mandal baada ya kupata matatizo ya shinikizo la damu. “Ni kweli amesitisha safari baada ya kuugua ghafla akiwa katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere, isipokuwa anaendelea vizuri na matatibabu,” alisema Jussa jana alipozungumza na vyombo vya habari kuthibitisha taarifa za Maalim Seif kuugua ghafla juzi. Jussa alisema baada ya mwanasiasa huyo maarufu visiwani kufikishwa katika hospitali hiyo madaktari bingwa walichukua vipimo muhimu kabla ya kuamuliwa kumlaza. “Tayari madaktari wameshachukua vipimo muhimu ingawa tatizo linalo msumbua ni presha, lakini anaendelea vizuri na matibabu,” alisema Mkurugenzi huyo. Hata hivyo, Daktari anayemtibu kiongozi huyo, Dk. Ramaiya Kaosheki, alipotakiwa kueleza maendeleo ya mgonjwa wake, alisema hawezi kuzungumzia ugonjwa unaomsumbua Maalim Seif. “Bado amelazwa na anaendelea kupata matibabu ingawa siwezi kusema anasumbuliwa na maradhi gani ningependa hilo umuulize msaidizi wake,” alisema Dk. Kaosheki . Taarifa kutoka Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere zimeeleza kuwa Maalim Seif alilazimika kukimbizwa hospitali baada ya afya yake kubadilika ghafla na mwili kuanza kupoteza nguvu wakati akisubiri kuanza safari yake ya Oman. “Naweza kusema hali yake haikuwa ya kawaida kabla ya kuanza kupatiwa matibabu na baadaye madaktari kuamua alazwe ili apate matibabu zaidi,” kilieleza chanzo kimoja cha habari.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote