Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, March 29, 2010

Balaa lingine Mara!

AJUZA mwenye miaka kati ya 90-100 Sifia Makubo amenyofolewa miguu yake yote miwili kwa panga na sasa yupo hospitali akiwa mahtuti. Ajuza huyo alikumbwa na mkasa huo mwishoni mwa wiki nyumbani kwake Ngerengere kata ya Sirari tarafa ya Inchugu wilayani Tarime Mkoani Mara. Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Tarime /Rorya Costantine Massawe alisema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 27 mwaka huu na ajuza huyo amelazwa katika Hospitali ya Wilaya Tarime. Imedaiwa kwamba ukatili huo amefanyiwa na Mkazi wa kijiji cha Kubiterere ambaye hakufahamika jina lake mara moja. Kamanda Massawe akielezea mkasa huo zaidi alisema mtuhumiwa huyo akiwa na panga alivamia nyumba ya bibi Huyo na kuanza Kumshambulia kwa Kumkata kata mapanga na kumwacha akivuja damu nyingi huku akilia kuomba msaada , Kamanda Massawe alisema kuwa Mjukuu wa Bibi huyo alisikia kilio cha bibi yake kuomba msaada na kuanza kupiga yowe ambapo wananchi Majirani walijitokeza mara moja na kumfukuza hadi walipomtia mikononi na kuanza kumpiga. Mtuhumiwa huyo alikatwa panga tumboni hadi utumbo wote kutoka nje. Polisi Kituo cha Sirari walifika waliwahi kufika kwenye kituo kumuokoa mtuhumiwa kwa kumfikisha hospitalini na ajuza huyo. Mtuhumiwa alifariki siku hiyo hiyo na ajuza huyo bado amelazwa Wodi namba 6 kwa matibabu ya miguu yake yote Miwili na majeraha ya mkono wa kushoto.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote