Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, March 3, 2010

Mamlaka yachunguza ajali ya ndege

MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imetuma timu ya wataalamu jijini Mwanza kuchunguza chanzo halisi cha ajali ya ndege aina ya Boeing 737 -200 namba BH-MVZ ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL). Aidha, Mamlaka hiyo imetangaza kuufunga uwanja wa ndege wa Mwanza kwa muda kwa ndege zote kubwa, hadi ndege hiyo itakapoondolewa eneo la tukio. Mkurugenzi wa Udhibiti wa Usafiri wa Anga wa Mamlaka hiyo, John Njau, alisema jana Dar es Salaam kuwa mpaka sasa haijafahamika chanzo hasa cha ajali hiyo, ambayo ilisababisha ndege hiyo kuharibika hasa kwenye mguu wake wa kushoto. “TCAA tumetuma wataalamu wetu kuchunguza chanzo cha ajali, na watachokifanya ni uchunguzi wa awali kwa kuhoji marubani, abiria na mashuhuda, uchunguzi huo utatuwezesha kuiondoa ndege hiyo eneo la tukio na hivyo kufungua uwanja,” alisema Njau. Alisema wataalamu wawili ndio waliokwenda kuchunguza tukio hilo ambao ni rubani mkaguzi na mhandisi mkaguzi, ambao wataungana na timu ya wataalamu wengine wakaguzi kutoka idara za usafiri wa anga kuchunguza tukio hilo. Alisema mamlaka hiyo ina taarifa kuwa ndege hiyo ilipatwa na tukio la hatari juzi asubuhi wakati ikiwa katika mkimbio wa kusimama na kutokana na mvua ilitoka kwenye njia na kuingia kwenye ardhi tifutifu na wakati ikiendelea na mwendo huo, tairi lilirudi ndani na pua ya ndege kugusa chini. Alisema watu wote 46 wakiwamo wafanyakazi saba wa ndege hiyo walitoka salama. “Napenda kusisitiza kuwa ndege hii haikuanguka bali ilipatwa na tukio la hatari tu na mguu wake mmoja umeharibika vibaya, tunataka kujua sababu halisi.” Alisema TCAA imelazimika kufunga uwanja huo kwa ndege kubwa hasa zinazoweza kutumia umbali wa meta 2,000 hata kusimama kutokana na ndege hiyo ya ATCL bawa lake kuwa katikati ya njia ya ndege na hivyo kuruhusu ndege zinazotumia umbali wa meta 1,800 tu kusimama. Hata hivyo, hakusema uchunguzi huo utachukua muda gani ili kuwezesha uwanja huo kufunguliwa. “Siwezi kusema ni lini tutamaliza kuchunguza na kuiondoa ndege hii, siwezi kusema leo, kesho au keshokutwa.” Naye Meneja Masoko wa ATCL, Musyangi Kajeri, alisema kampuni hiyo pia imetuma wataalamu wake kuchunguza tukio hilo na kuangalia uwezekano wa kuendelea na huduma zake kama kawaida. Ndege hiyo ilipatwa na mkasa huo juzi asubuhi ikitoka Dar es Salaam kwenda Mwanza na wakati wa kutua ilivamia maji yaliyotokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha Mwanza ambayo kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi wa ATCL, William Haji, yaliingia kwenye injini moja na ilizima ghafla na kusababisha mtafaruku huo. ( Chanzo cha habari - Habari Leo)

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote