Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, March 25, 2010

Ajali Mbaya - Kibamba

Kuna habari za kuaminika kuwa kuna Hiace lenye no ya usajili T615 AJW lililokuwa linatokea Ubungo kwenda Mlandizi imegongwa uso kwa uso na Lori la mafuta aina ya Scania lenye no za usajili T192ABP iliyoandika kwa nyuma maandishi yanayosomeka (Yarabi salama)majira ya saa 1 asubuhi ya leo eneo la Kibamba - Morogoro Rd, Dar es Salaam. Ni ajali mbaya na ya kutisha , mmoja wa mashuhuda kashuhudia maiti zisizopungua saba kwenye Hiace na kaongeza kwa kasema kuwa "Scania imeilalia hiace kabisa yaani scania iko juu hiace iko chini hata kuokoa haiwezekani..na sidhani kama kuna mtu atakuwa amepona ila kwenye scania dereva na konda anaweza akawa amepona..sikuwa na kamera ningeweka kupiga picha, Zimamoto wameelekea eneo la tukio . Taarifa zaidi na za kuaminika tutawaletea baadae . Mungu atupe subira na Uvumilivu

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote