Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, March 15, 2010

Pengo azindua hospitali Kibangu

ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amezindua Hospitali ya Misheni ya Kibangu na kuwahimiza waumini wenye uwezo kujitolea kuchangia katika ujenzi wa Hosptali hiyo ili kusaidia kufikisha huduma za afya kwa jamii. Hospitali hiyo ambayo ina ghorofa mbili na tayari imesajiliwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii namba yake ikiwa 071350 tayari imeanza kuanza kuhudumia wagonjwa huku ujenzi wake uliosimamiwa wa Kanisa hilo Parokia ya Kibangu hadi sasa umeghalimu zaidi ya Sh 482.6 milioni. Katika hotuba yake ya uzindizi Pengo aliwahimizi waumini na watu wenye uwezo kuwa na moyo wa kujitolea katika michango ya ujenzi wa hospitali hiyo kwa kufanya hivyo kutawafanya washiriki kazi ya uponyaji iliyofanywa na Yesu Kristu. Tunapojenga hospitali kama hii tunawalenga watu ambao uwezo wao ni pungufu hasa akinamama, ili waweze kupata huduma hizi muhimu kwa ustawi wa maisha yao. Ninasema hivi kwa sababu watu wenye uwezo mkubwa huweza kuzipata huduma hizi kokote , kwa gharama yoyote na wakati mwingine huzifuata hata nje ya nchi kama Afrika ya kusini Ulaya na sehemu nyingine,alisema Pengo. Alisema watu wenye uwezo ni vyema wajitolee katika kuchangia huduma na ujenzi wa hospitali hiyo akiongeza kuwa huduma zake hazibagui dini, kabila wala rangi na kusisitiza kwamba ina lengo la kusaidia watu eneo hilo ambao kwa muda mrefu walikuwa wakimihaha kupata huduma hizo. Naye mwenyekiti wa Parokia hiyo Adrian Mpande alisema, ukosefu wa hospitali katika eneo hilo uliodumu kwa muda mrefu aliwalazimu watu kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya wanapougua. Mpande alifafanua kuwa mradi wa hospitali hiyo ulibuniwa mwaka 2003 na ambapo gharama za ujenzi wake zilikadiriwa kuwa Sh305 milioni lakini, baaaye zilipanda hadi kufikia sh 461 milioni katika mwaka 2008 na sasa hadi kukamilika kwake kutumika sh 500 milioni. Alisema hospitali hiyo hadi sasa inauwezo wa kulaza wagonjwa 50 kwa wakati mmoja na inatoa vipaumbele kwa wakinamama wajawazito,watoto na kiliniki za kwa jili ya kupima virusi vya Ukimwi.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote