Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, March 3, 2010

Msiba mkubwa Tabora

IDADI ya watu waliokufa kwenye ajali ya basi la AM Coach iliyotokea jumapili wilayani Nzega, imefikia 26, baada ya wengine wawili kufariki dunia juzi, huku maiti 18 wakitambuliwa na ndugu zao. Kutokana na kutambuliwa kwa miili hiyo, hadi kufikia juzi mchana, maiti wanane walikuwa hawajatambuliwa na wanaendelea kuhifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Nzega, kutokana na marehemu hao kutokuwa na vitambulisho vyovyote. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Liberatus Barlow, maiti hao 18 walitambuliwa kwa vitambulisho vya kazi, vya kura na kadi za benki. Kamanda Barlow aliwataja waliotambuliwa hadi juzi kuwa ni Faustine Simon wa Katesh, Manyara; Pastory Kaiza; Epelanya Mleke; Gerald Nyitwe ambaye ni askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Kikosi cha 39 Arusha; Julieth Rupia wa Mwanza na Stephen Malolo wa Shinyanga. Wengine ni Noel Munisi; Paul Boniface wote wa Manyara; Ritha Thomas wa Moshi; Magreth Asenga (Moshi); Elizabeth Uriki ambaye ni Mtawa wa Kanisa Katoliki (Mwanza); Salome Richard (Babati); Doria Agai (Mwanza); Joachim Paul (Nzega); James Agai (Mwanza); Abeid Ngayanimo (Nzega), Milambo Benjamin (Nzega) na Benson Ochieng. Aidha, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Nzega, Dk. John Mombeki, alisema majeruhi wanne waliovunjika miguu na mikono walikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza kwa tiba zaidi baada ya madaktari wa hospitali hiyo kukosa uwezo wa kutoa matibabu zaidi kwa majeruhi hao. Aliwataja majeruhi waliokimbizwa Bugando kuwa ni Nakijiwa Ibinga wa Same Kilimanjaro; Prosper Magacha (Hanang); Joyce Nyanda (Nyakato - Mwanza) na Chega Msila (Mwanza). Dk Mombeki alisema majeruhi wengine wawili waliokuwa wakikimbizwa pamoja nao kwenda Bugando, walifariki dunia njiani, hivyo kufanya idadi yao kuwa 26 baada ya juzi watu 24 kufa papo hapo katika ajali hiyo iliyotokea kati ya Kitangiri na Migua kiasi cha kilometa 12 kutoka Nzega mjini. Alisema kulingana na taarifa za kitabibu, majeruhi wengine sita wanatarajiwa kusafirishwa kwenda Bugando kwa matibabu zaidi. Akizungumzia majeruhi waliobaki hospitalini hapo, Mganga Mkuu wa Wilaya alisema wanaendelea vizuri na wamekuwa wakipata tiba kama inavyotakiwa na wakiendelea hivyo, wataruhusiwa kutoka siku chache zijazo. Katika hatua nyingine, imebainika kuwa mtoto ambaye hajatambuliwa jina, ni miongoni mwa majeruhi waliofikishwa hospitalini hapo kupatiwa matibabu. Dk Mombeki alisema mtoto huyo amepewa uangalizi maalumu kutokana na umri wake kuwa mdogo kuliko wote walionusurika katika ajali hiyo na afya yake inaendelea vizuri. Inahisiwa kuwa mzazi au mlezi wake aliyekuwa akisafiri naye kwenye basi hilo alipoteza maisha. Alisema pamoja na mtoto huyo, pia watoto wengine mapacha wenye umri wa mwaka mmoja wamenusurika na wamelazwa hospitalini hapo. Mganga Mkuu aliwataja watoto hao kuwa ni Brighton na Brightness Juma ambao wanaishi na wazazi wao Mwanza ambapo pia mtoto mwenye umri wa miaka miwili, Mary Ochieng alinusurika. Hii ni ajali ya kwanza kutokea Tabora mwaka huu na kuua idadi kubwa ya watu aidha, ni ajali ya pili kubwa mwaka huu baada ya mabasi ya Chatco na Mzuri Trans kugongana uso kwa uso katika kijiji cha Kwangahu Handeni, Tanga na kuua watu 26.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote