Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, March 31, 2010

CCJ yapokea kigogo wa CCM

JANA mbunge wa jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga, Bw. Fred Mpendazoe ametangaza rasmi kujiengua CCM na kujiunga na Chama cha Jamii CCJ. Hivyo kutokana na maamuzi hayo chama hicho kipya cha jaamii kilichotangaza awali kuwa kuna vigogo wa CCM watakifata chama hicho hivyo imethibitisha kauli hiyo baada ya mbunge huyo kuwa wa kwanza kujiengua na CCM na kujiunga huko.Alisema amejiengua na CCM ili kuweza kutetea maslahi ya wananchi wanyonge ambapo ameona ndani ya CCM jambo ambalo halitaweza kutekelezwa kwa kuwa kila mtu anatetea masilahi yake binafsi na si kutazama wananchi wapiga kura.Alifafanua kuwa serikali inayoundwa na CCM inayumba kwa kushindwa kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu sakata hilo la Richmond ambalo lilihusisha serikali kuipa zabuni ya kufua umeme wa dharura kampuni hiyo bila kufuata Sheria ya Manunuzi ya Umma, kashfa ya mgodi wa Kiwira kuuzwa kwa bei nafuu na mkataba wa uendeshaji wa Shirika la Reli (TRL) ambao umezorotesha kabisa huduma za reli ya kati. Hivyo kwa kujiunga kwake ataweza kurekebisha mambo hayo kwa kujiunga na chama hicho.Alisema CCM imetekwa na wafanyabishara wanaojikita katika kuwania nyadhifa mbalimbali kwa lengo la kuficha maovu yao badala ya kuwatetea wananchi"Nimeishi kwa matumaini ndani ya CCM kwa muda mrefu na sasa natangaza wazi kuwa nakihama chama hicho na kuhamia chama mbadala ambacho ni CCJ," alisema Mpendazoe

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote