Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 23, 2010

Wanafunzi IFM wagoma kupinga ongezeko la ada

WANAFUNZI wa Shahada ya kwanza na ya pili katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha [IFM] jana waligoma kuendelea na masomo kutokana na ongezeko la ada lililopanda ghafla. Wanafunzi hao jana waliamua kuweka mgomo baada kupinga ongezeko la ada zaidi ya asilimia 50% .Walionekana kuandamana kwenda kutaka kumuona mfadhili wa chuo hicho ambae ni Waziri wa Fedha ili wamueleze tatizo hilo kama ana taarifa nalo.Wanafunzi hao waliweka mgomo huo baada ya kutopata majibu ya matokeo ya mitihani baada ya kuambiwa hadi wamalize ada na kushangazwa na kauli hiyo.Wanafunzi hao walidai kuwa ada zimepanda kutoka shilingi milioni moja hadi kufika milioni moja na laki sita jambo ambalo limewashangaza kupanda kwa ada hizo bila ya kupewa taarifa rasmi.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote