Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, March 8, 2010

Michael Owen Kukaa nje msimu mzima!

Mshambulizi wa klabu ya soka ya Manchester United ya Uingereza, Michael Owen, akiwa na matatizo ya misuli ya paja, tangu mechi ya ushindi wa magoli 2-1 ya Kombe la Carling dhidi ya Aston Villa, hataweza kucheza tena msimu huu. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30, alifunga bao la kusawazisha katika mechi hiyo ya Wembley, lakini alipatwa na matatizo ya misuli alipokuwa akiukimbilia mpira katika kipindi cha kwanza. Kujeruhiwa kwa Owen kumempotezea matumaini yote ya kushirikishwa katika timu ya England. Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amesema kwamba kinyume na walivyofikiria hapo awali, hali ya Owen ni mbaya zaidi, na kwa kiasi fulani, alisema huenda hayo yalitokana na uwanja wa Wembley. Owen, ambaye ana mwaka mmoja uliosalia katika mkataba wake wa miaka miwili na Man U, awali alitazamiwa kupumzika kwa wiki chache tu. Atafanyiwa upasuaji Jumatatu.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote