Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 16, 2010

Ali Ameir kung`atuka ubunge

Mwanasiasa mkongwe Zanzibar, Ali Ameir Mohammed, ametangaza kung’atuka kuwania ubunge katika uchaguzi mkuu ujao. Ali Ameir ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Donge, Kaskazini Unguja, amewahi kushika nyadhifa mbalimbali katika Serikali ya Muungano pamoja na Chama cha Mapinduzi (CCM). Amesema ameamua kutogombea tena ubunge ili apumzike. Alisema uamuzi huo ni wake binafsi na kwamba hakuna kituo chochote kilichotaka aendelee kuwa mbunge wao.Alisema wananchi wa Donge bado wana imani na utumishi wake na hata kama wangejitokeza wanachama 100 kupambana naye angeweza kushinda. Alisema tayari wazee wa Donge wamekubali uamuzi wake wa kutogombea ingawa kwa kinyongo. Hata hivyo alisema uamuzi wake wa kustaafu huuna nia ya kuwashawishi wazee wengine kufuata nyayo zake kwa kuwa suala hilo ni hiari ya mtu. Miongoni mwa nyadhifa alizowahi kushikilia Mbunge wa jimbo hilo ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Mshauri wa Rais wa Zanzibar wa masuala ya siasa, Waziri wa Habari na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Ameir ni mwanasiasa wa pili mkongwe kutangaza uamuzi kama huo Zanzibar. Mwingine ni Mbunge wa Makunduchi, Abdusalami Isaa Khatib, ambaye ameshasema kuwa hatagombea mwaka huu. Khatib hivi sasa ni Mbunge wa Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja.

Chanzo: Nipashe

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote