Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, March 31, 2010

Mama Kikwete anusurika katika ajali Mara

MKE wa Rais Mama Salma Kikwete anusurika kifo kwa ajali mbaya baada ya msafara wake kuingia doa kwa kuvamiwa na lori na kugonga magari matatu ya msafara huo. Ajali hiyo ilitokea jana wilayani Rorya mkoani Mara wakati Mama Salma akiwa ziarani mkoani humo. Kamanda wa Polisi Tarime, Bw. Constantine Masawe alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na alisema lori hilo lilisimamishwa na askari wa barabarani lisimame ili kupisha msafara huo na kukaidi na kuingia barabarani na kusababisha ajali hiyo.Amesema kuwa lori hilo liligonga magari matatu ya nyuma ya msafara huo na kusababisha ajali ambayo haikuwa ya lazima kwa muda huo.Amesema lori hilo lilikuwa linatokea nchini Kenya ambapo ilidaiwa pia lori hilo lilikuwa limebeba mali za magendo.Hivyo imedaiwa dereva huyo ameshikiliwa na jeshi hilo ili kujibu tuhuma hizo.Hata hivyo hakuna aliyeweza kupoteza maisha katika ajali hiyo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote