
Mtoto mmoja wa Kiume nchini China ambaye amezaliwa akiwa na jumla ya Vidole 31 amefanyiwa operation wa kutolewa vidole vya ziada , Inasemekana kuwa operation hiyo iliyodumu kwa masaa 6 1/2 ilifanyika katika Hospitali ya Shengjing huko Shenyang China, katika Operation hiyo Madaktari walifanikiwa kutoa vidole 11 vya ziada ambavyo baadhi ya vidole vya mikono vilikuwa vimeungana .Kutokana na maelezo ya mama wa mtoto huyo , mwanawe alipachikwa jina la "Monster" na watoto wenzake darasani (chekechea) na inasemekana kuwa akawa mtu wa kwanza kuwa na Vidole vingi duniani kwa madai ya Gazeti la Daily Mail. Moja ya mguu wake ulikuwa na vidole 7 na mwingine 8, mkono mmoja ulikuwa na vidole 3 vilivyoungana na mwingine ukiwa na 4 vilivyoungana pia.
No comments:
Post a Comment