Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 16, 2010

Aona kwa kutumia ulimi

TATIZO la upofu sasa linaweza kuwa historia baada ya wanasayansi kuanza kumfundisha mwanajeshi wa Uingereza ambaye alipofuka vitani, kuona kwa kutumia ulimi wake. Craig Lundberg, 24( pichani), ambaye alipoteza uwezo wake wa kuona baada ya kupigwa na kombora la roketi miaka mitatu iliyopita, ni mwanajeshi wa kwanza kujaribishiwa teknolojia hiyo inayoitwa mfumo wa BrainPort, kwa mujibu wa Skynews. Kifaa hicho kinachotumika kumuwezesha mtu kuona kinahusisha teknolojia ya hali ya juu ya 'lollipop' ambayo imewekwa kwenye ulimi wa Craig. Kifaa hicho kinabadilisha picha kutoka kwenye kamera ya video, ambayo inavaliwa kwenye miwani, kuwa ishara ambayo huchangamsha seli zilizo kwenye lollipop. Kifaa hicho cha thamani ya Pauni 10,000 za Kiingereza kinatumia kanuni ya hisia mbadala. Ubongo hutambua kuwa ishara hizo zinazousisimua ulimi, hazina uhusiano na ladha na hivyo kuzielekeza kwenye sehemu ya picha katikati ya akili kwa ajili ya kuitengeneza taswira hiyo. Akili huweza kutafsiri picha hiyo na hivyo kumpa Craig uwezo wa kuona. Craig anaeleza kifaa hicho kuwa ni "kizuri cha aina yake". "Kila kitu ambacho kamera inaangalia, nahisi picha kwenye ulimi wangu," alisema. Mfumo huo pia unamuwezesha kutambua herufi. Alisema: "Naweza kuhisi kwa kutumia ulimi wangu kuwa herufi ya kwanza ni A na baadaye naelekea kwenye herufi inayofuata. Ni kitu cha ajabu. "Baadaye natembea kwenye varanda na naweza kwenda milangoni, ukutani na kuona watu wanaokuja kwangu." Teknolojia hiyo ya Lundberg ya BrainPort imefadhiliwa kwa pamoja na Wizara ya Ulinzi na taasisi ya hisani ya askari vipofu. "Mimi ni mkweli," alisema. "Najua hii haitanirejeshea kabisa uwezo wangu wa kuona, inaweza kuwa kitu kizuri kinachofuata."

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote