Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 16, 2010

MV Serengeti yateketea kwa Moto

Meli ya MV Serengeti imeteketea kwa moto siku ya jumapili na mabaharia wanane wamenusurika kufa, wakati ikiwa imetia nanga nje ya bandari ya Malindi mjini Zanzibar. Moto huo ulianza kuwaka majira ya saa 6:30 mchana na kusababisha wasiwasi mkubwa katika eneo hilo lenye ukanda wa hoteli nyingi za kitalii, baada ya umati wa watu kuvamia maeneo hayo wakitaka kushuhudia moto huo. Mrajisi wa Meli Zanzibar, Abdallah Mohammed, alisema kwamba moto huo hadi juzi mchana ulikuwa unaendelea kuzimwa kwa kutumia Tagi ya Shirika la Bandari Zanzibar (ZPC), pamoja na vifaa vya uokoaji kwenye majanga ya moto vilivyomo ndani ya meli hiyo. Hata hivyo, alisema ni mapema kueleza mabaharia wangapi walikuwemo ndani ya meli hiyo na chanzo cha moto huo, hadi hapo uchunguzi wa kitaalam utakapofanyika. Mohamed alisema meli hiyo inamilikiwa na kampuni ya JAK Enterprises L.T.D iliyosajiliwa Zanzibar na kwamba kwa mara ya mwisho ilifanyiwa ukaguzi kati ya Januari na Desemba mwaka jana. “Ukaguzi wa mwisho ulionyesha meli ni nzima na ndiyo maana ikaruhusiwa kutoa huduma ya kubeba abiria na mizigo” alisema Mrajisi huyo wa meli. Alieleza kwamba leseni ya meli hiyo inaruhusu kubeba abiria 550 na tani 100 za mizigo na ilikuwa ifanye safari jana usiku kuelekea kisiwani Pemba. Alisema hilo ni tukio la pili la meli za abiria kuungua moto zikiwa zimeshusha nanga nje ya bandari ya Malindi, ambapo hivi karibuni meli za MV Aziza I na Aziza II ziliteketea kwa moto wakati zikifanyiwa matengenezo katika eneo la Mtoni, nje kidogo ya Bandari ya Malindi. Hata hivyo, alisema kwa mujibu wa sheria abiria wote waliokuwa wasafiri na meli hiyo jana usiku wanapaswa kurejeshewa fedha zao au watafutiwe usafiri mwingine wa kuwafikisha. Kwa upande wake, Mkuu wa Operesheni wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar, alisema ni mapema kuelezea chanzo cha moto huo na mabaharia waliokuwemo hadi hapo kazi ya uokoaji itakapokamilika. “Ni mapema kusema chanzo cha moto isipokuwa hatua za uokoaji zinaendelea na sehemu kubwa ya moto imekwisha dhibitiwa”, alisema Mkuu huyo wa Opereshen.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote