Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 23, 2010

Hatima ya LIYUMBA Ni April 9 ,Mahakama yaombwa kutupilia mbali kesi inayomkabili

JOPO la mawakili wanne wanaomtetea, Mkurugenzi wa zamani wa Utawala na Fedha wa BoT, Amatus Liyumba wamewasilisha hoja za majumuisho za mwisho wakiitiaka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imuone mteja wao hana kesi ya kujibu dhidi ya mashtaka yanayomkabili. Kigogo huyo wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba anakabiliwa na kesi ya kuisababishia serikali hasara ya Sh 221. Ilielezwa kuwa Aprili 9, mwaka huu, hatma yake itajulikana kama hana kesi ya kujibu ama la. Hatua hiyo imekuja baada ya upande wa mashtaka Machi 15, mwaka huu kufunga ushahidi wao mbele ya jopo la mahakimu watatu lililokuwa likiongozwa na Hakimu Edson Mkasimongwa. Wakili wa Serikali Juma Mzarau alifunga ushahidi huo baada ya mashahidi wao nane kutoa ushahidi dhidi ya kesi hiyo kati ya mashahidi 15 waliotarajia kuwaita. Wakiwasilisha hoja hizo za mwisho za majumuisho kwa njia ya maandishi, mawakili wa Liyumba, Hilary Mkate, Majura Magafu, Hudson Ndusyepo na Onesmo Kyauke waliiomba mahakama imwone mteja wao hana kesi ya kujibu kwa madai kuwa ushahidi uliotolewa na mashahidi nane wa upande wa mashtaka hautoshelezi kuithibitishia mahakama kwamba Liyumba alitumia vibaya madaraka yake kinyume na sheria, chini ya kifungu cha sheria cha 96 (i) cha kanuni ya adhabu. Walidai katika majumuisho hayo Shahidi wa nane na wa saba wa upande wa mashtaka walieleza katika ushahidi wao kuwa ni vigumu kuthibitisha hasara inayodaiwa kusababishwa na Liyumba kwa sababu ripoti kamili ya utekelezaji wa mradi wa Mtemi Mirambo unaojulikana kama Majengo Pacha hadi sasa bado haijaandaliwa. Kutokana na ushahidi huo, Mawakili hao, waliitaka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imwone Liyumba kuwa hana kesi ya kujibu kwa sababu hakuna uthibitisho wowote ambao unaonyesha kuwa serikali imepata hasara katika mradi huo. Mawakili hao wa Liyumba waliongeza kudai kuwa ni mapema sana kudai kuwa serikali imepata hasara katika mradi wa majengo Pacha bila ya kuandaliwa kwa ripoti kamili ya mradi huo. Walidai kuwa licha ya upande wa mashtaka kushindwa kuithibitishia mahakama kuwa Liyumba alifanya maamuzi yenye madhara katika mradi wa majengo pacha, pia umeshindwa kuthibitisha kwamba Liyumba alifanya maamuzi hayo kwa nia ovu. Mawakili hao walisisitiza mahakama imwone mteja wao hana kesi ya kujibu na iliomba iyatupilie mbali mashtaka yanayomkabili mteja wao huyo.
Chanzo : Mwananchi

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote