Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, March 24, 2010

Mapenzi yampeleka Kaburini yeye na mtoto wake

Katika hali ya kusikitisha, mwanaume aliyetambuliwa kuwa ni Mwidadi Hamisi,(32) mkazi wa Bombambili mjini Songea, mkoani Ruvuma, amemnyonga mtoto wake wa umri wa miaka minne na baadaye naye kujinyonga huku akiwa ameacha ujumbe kuwa uamuzi huo umetikana na shida alizokuwa akipata kutoka kwa mke wake wa zamani.Tukio hilo lilisikitisha wengi hasa kwa kitendo cha kumnyonga mtoto Mulla, ambaye hakuwa na hatia, lilitokea saa 5:00 asubuhi wiki iliyopita katika maeneo ya Mlima wa Chandamali,nje kidogo wa mji wa Songea.Kabla ya kuamua kujinyonga, marehemu ambaye wakati wa uhai wake alikuwa mwendesha pikipiki zinazosafirisha watu,alimpiga simu kwa tajiri wake akimtaka afuate pikipiki yake katika maeneo ya mlimani huo.Habari zilisema katika simu hiyo marehemu alimwambia tajiri yake kuwa yeye ameamua kwenda kupumzika kaburini na mtoto wake, ili kuepuka shida alizokuwa akizipata kutoka kwa mke wake wa zamani.Kabla ya kujinyonga, Mwadadi, aliacha ujumbe huku akiambatanisha na orodha ya namba za simu za ndugu zake na kutaja sehemu anakotoka kuwa Newala mjini mkoani Mtwara.Katika ujumbe huo, marehemu alisema ameamua kujinyonga yeye na mtoto wake kufuatia kashfa alizokuwa akizipata kutoka kwa mama watoto wake.Katika ujumbe huyo marehemu alimtuhumu mama huyo kuwa amekuwa akimweleza mpenzi wake, siri za maungoni mwake.Akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio tajiri wa marehemu huyo,Hussein Msafiri, alisema siku kadhaa zilizopita, marehemu aliwahi kumweleza matatizo yake yeye na mke wa zamani."Mara nyingi alionekana mtu ambaye hana amani moyoni mwake," alisema

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote