Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, March 25, 2010

23 Wanusurika kwenye ajali ya basi la HEKIMA

WATU 23 wamenusurika kupoteza maisha baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupinduka katika kijiji cha Tanangozi, mkoani Iringa. Ajali hiyo ilitokea jana saa tano asubuhi, baada ya basi la Hekima kulipita gari ndogo lililokuwa limebeba pombe ya kienyeji aina ya ulanzi kisha kuserereka na kupinduka. Basi hilo lililokuwa na abiria zaidi 70 lilikuwa likitoka Mbeya kwenda Dar es Salaam. Akizungunza na vyombo vya habari kwa njia ya simu, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa, Dk George Kabona alisema kati ya majeruhi hao, 13 ni wanaume na kumi ni wanawake na kwamba hali ya majeruhi mmoja ikiwa ni mbaya. "Majira ya saa 6 mchana leo (jana), tulipokea majeruhi 23 kutoka katika ajali ya basi iliyotokea katika kijiji cha Tanangozi. Kati ya hao 13 ni wanaume na kumi ni wanawake na hali zao zinaendelea vizuri, lakini mmoja kati yao hali yake ni mbaya na amelazwa chumba cha wagonjwa mahututi," alisema Dk Kabona. Dk Kabona alisema kuwa kwa mujibu wa majeruhi hao, ajali hiyo ilitokea kutokana na barabara katika eneo hilo kuwa na utelezi uliosababishwa na mvua nyingi zinazoendelea kunyesha mkoani Iringa na mikoa mingine katika Nyanda za Juu Kusini. Alisema kwamba baada ya basi kulipita gari dogo lililokuwa limebeba pombe aina ya ulanzi na dereva kutaka kurudi katika njia yake ndipo liliposerereka na kupinduka. Mmoja wa majeruhi hao alipouliza alisema kuwa ajali hiyo ilitokea baada ya basi (Hekima) kulipita gari dogo lililokuwa limebeba pombe ya ulanzi na kuserereka kutokana na barabara kuwa na utelezi uliosababishwa na mvua," alibinisha Dk Kabona.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote