Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 16, 2010

KenolKobil kununua mali za BP Tanzania

Kampuni ya KenKobil ambayo hujishughulisha na biashara ya uuzaji mafuta, inakusudia kununua mali ya Kampuni ya BP Tanzania Limited ambayo hivi karibuni imetangaza kuachana na biashara ya mafuta katika nchi tano za Afrika ambazo ni Tanzania, Zambia, Namibia, Botswana na Malawi. Taarifa iliyotolewa na mmoja wa mameneja wake, Patrick Kondo, imeeleza kwamba KenolKobil, imevutiwa kuchukua nafasi ya masoko ambayo BP Tanzania Limited inataka kuachia kwa sababu kampuni hiyo ilikuwa na uendeshaji mzuri wa biashara zake na ilikuwa na masoko ya uhakika katika nchi zote tano. “Pia BP Tanzania inayo miundombinu mizuri na iliyojengeka vizuri katika nchi zote hizo ambayo inaachia, vile vile ilikuwa na inadhibiti sehemu kubwa ya soko miliki na uendeshaji thabiti wa shughuli zake,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo. Pia meneja huyo alisema KenolKobil imevutiwa zaidi na masoko hayo na nafasi kubwa ya kibiashara inayotoa kwa uwezekano mkubwa wa kukua kwa kampuni hiyo barani Afrika, hasa ikizingatiwa na “Mkakati Kuelekea Kusini” kama ilivyotangazwa mwaka jana. “Masoko haya yote yako katika maeneo ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika ambako masoko ya KenolKobil ambayo Bodi ya KenolKobil imeyaridhia kwa lengo la kuwekeza. KenolKobil inaouweza wa kifedha kununua sio mali hizo tu, bali hata nyinginezo,” alisema. Alisema miongoni mwa masoko hayo, Tanzania na Zambia, KenolKobil tayari ina makampuni yake tanzu na inao mpango wa upanuzi na kuimarisha biashara zake kwenye masoko hayo kwa kulingana na madhumuni na malengo ya kutaka kuwa kiongozi katika kila soko na mfanyabiashara mkubwa barani Afrika. Alisema KenolKobil inatambua kuwa masoko yote ambayo BP imetangaza kujitoa, kuna mwelekeo mzuri wa ukuaji wa biashara ambao utatoa fursa nzuri kwa kampuni yetu kuweza kuongeza biashara kulingana na malengo yetu.
Chanzo: Nipashe

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote