Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 16, 2010

Mtu Mfupi kuliko wote Duniani afariki

He Pingping ambaye aliyekuwa akitambulika kama mwanaume mfupi kuliko wote duniani akiwa na urefu wa sentimeta 74.61 amefariki dunia jumamosi kutokana na matatizo ya moyo. He Pingping, amefariki dunia nchini Italia akiwa na umri wa miaka 21.He alikuwa nchini Italia kwa ajili ya kushiriki kwenye shoo ya kwenye luninga lakini alisumbuliwa na maumivu makali kwenye kifua na alipowahishwa hospitali wiki mbili zilizopita alifariki siku ya jumamosi kutokana na kile kinachoaminika kuwa ni matatizo ya moyo.He alizaliwa nchini China akiwa na ugonjwa unaomfanya awe mfupi sana. Baba yake He Yun aliwahi kusema kuwa He alipozaliwa alikuwa mdogo sana kiasi cha kuenea kwenye viganja vyake vya mikono.He alitambulika rasmi kama mtu mfupi duniani na kuingizwa kwenye kitabu cha rekodi za dunia, Guinness mnamo mwaka 2008.Akiwa na taji lake hilo, He alisafiri nchi mbalimbali duniani kutangaza rekodi yake hiyo akiwa na watu wengine waliovunja rekodi za dunia.Mwezi septemba mwaka 2008, He alienda mjini London, Uingereza na kupiga picha na mwanamke mwenye miguu mirefu kuliko wanawake wote duniani, Svetlana Pankratova.Mwanzoni mwa mwaka huu, He alisafiri kwenda Istanbul,Uturuki ambapo alikutana na mtu mrefu kuliko wote duniani Sultan Kosen mwenye urefu wa sentimeta 246.5.Guinness World Records wamesema kuwa mrithi wa taji la He atatangazwa katika siku zijazo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote