Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, March 22, 2010

Namibia wamkumbuka Nyerere

SERIKALI ya Namibia imemtunuku Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere nishani ya heshima. Nishani hiyo alikabidhiwa mkewe, Mama Maria ikiwa ni utambuzi na kuthamini nafasi yake katika harakati za kupigania uhuru wa Afrika ikiwemo nchi yao . Alikabidhiwa nishani hiyo juzi pamoja na watu wengine sita mashuhuri waliotoa mchango mkubwa kwa Namibia na kufanikisha ipate Uhuru Machi 21, 1990 kutoka kwa Afrika Kusini. Walipewa tuzo hizo wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na Rais Hifikepunye Pohamba kwa ajili ya marais wote na wageni wengine waalikwa waliofika nchini hapa, akiwemo Rais Jakaya Kikwete kushuhudia sherehe za miaka 20 ya Uhuru pamoja na kuapishwa kwa Rais na Waziri Mkuu nchini hapa. Akielezea umuhimu wa Namibia kumtunuku Mwalimu Nyerere, Msimamizi wa Itifaki katika hafla hiyo, Martin Anyamba alisema kuwa mamilioni ya Waafrika, jina la Nyerere litaendelea kuwa kwenye kumbukumbu zao na wataendelea kumheshimu. Alisema Nyerere alikuwa mwanafalsafa, kiongozi na kiunganishi cha watu na mtu mwenye busara aliyefanya kazi kubwa ya kufungua mipaka ya nchi yake kwa ajili ya kupigania uhuru wa nchi mbalimbali barani. Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na Rais Jakaya Kikwete, ilielezwa kwamba ushirikiano na umoja wa Namibia uliowezesha kupata uhuru, ulitokana na mchango mkubwa wa Tanzania ambayo ilijitoa mhanga kwa ajili yao . “Wanachama wengi wa SWAPO walipata mafunzo huko Kongwa ( Dodoma )…Mwalimu Nyerere alikuwa muumini mzuri wa umoja,” alisema Anyamba kabla ya kumuita Mama Maria aliyekuwa wa kwanza kati ya watu saba kutunukiwa, kitendo kilichoshangiliwa kwa makofi na vigelegele na umati uliohudhuria. Wengine waliokabidhiwa nishani hizo kutokana na mchango wao katika uhuru wa Namibia ni Rais Mstaafu wa Zambia , Kenneth Kaunda aliyekwenda kuipokea kwa mbwembwe akitembea kwa mwendo wa haraka. Wakati huohuo Umoja wa Wanawake Watanzania waishio Namibia kupitia kwa Mwenyekiti wao, Chiku Mnubi, juzi walimpa Mama Nyerere zawadi ya ramani ya nchi hiyo ikiwa ni utambuzi wa mchango wake katika uhuru na pia kumshukuru kufika nchini humo kuhudhuria sherehe za Uhuru na kuapishwa kwa Rais Pohamba.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote