Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, March 25, 2010

Mshindi wa Miss Universe 2009 alamba BINGO

MREMBO wa Tanzania, Miss Universe Tanzania 2009, Illuminata James, amepata fursa ya masomo scholarship nchini Marekani kutoka kwa Kampuni ya New York Film Academy. Mbali na kutoa nafasi hiyo ya masomo, pia kampuni hiyo imejitolea kudhamini mashindano hayo mwaka huu na kuahidi pia kutoa fursa ya masomo kwa mshindi atakayemrithi Illuminata. Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communication, ambao ndiyo waandaaji wa mashindano hayo taifa, Maria Sarungi, aliwaambia waandishi wa habari jana wameamua kuboresha mashindano hayo zaidi ikiwa ni sambamba na kutafuta udhamini wa nje ya nchi ili kuongeza chachu ya mashindano. Alisema kuwa hiyo itakuwa ni nafasi ya pekee kwa warembo wa Tanzania kujitokeza ili kuwania nafasi hiyo nyeti na nyingine nyingi ambazo wadhamini wa hapa nchini watatoa. "Tunatarajia kufanya usaili wa warembo hao katika mikoa mitano ya Tanzania Bara ambayo ni Mwanza, Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma na Arusha ili kupata warembo 20 ambao wataingia kambini kwa ajili ya kuchuana hadi kumpata mshindi. "Katika usaili huo tutaangalia zaidi vigezo ili kumpata mrembo bomba ambaye atatuwakilisha vema kimataifa na hatimaye kuibuka na ushindi" alisema Sarungi. Wadhamini wengine kwenye mashindano hayo ni Kampuni ya Precision Air, Serengeti Breweries, PSI, Movenpick Hotel, Hugo Domingo, Choice FM, Prime Time Promotions pamoja na Midland Hotel.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote