Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, March 25, 2010

Mvua Kubwa yatishia Mwanza

MVUA kubwa iliyonyesha jana alfajiri jijini hapa kwa saa mbili imezikosesha makazi zaidi ya kaya 24 za mtaa wa Mabatini Kusini na 10 za Mabatini Kaskazini. wakazi wa kaya hizo walionekana katika harakati za kukusanya vyombo na mali zao zingine zikiwa zimelowa maji na baadhi ya nyumba zikiwa zimebomoka. Akizungumza katika mtaa wa Mabatini Kusini, Mwenyekiti wa Mtaa huo, Yohana Nono, alisema msaada wa haraka wa mahema, vyakula na nguo unahitajika kuwasitiri baadhi ya wananchi ambao vitu vyao vilisombwa na mafuriko ya maji. “Baada ya kufanya tathmini na wananchi wa mtaa wangu, tumebaini kuna jumla ya watu 100 wa kaya 24 ambao nyumba zao zimebomolewa na mafuriko, “ alisema Nono na kuongeza kuwa wanafanya juhudi ya kuwasiliana na uongozi wa wilaya ili kuona uwezekano wa kuwasaidia wananchi hao. Kati ya watu walioathiriwa na mafuriko hayo ni pamoja na Stella Robert (6), ambaye kwa mujibu wa mjumbe wa nyumba 10 shina la Mabatini Kusini mtaa wa Benjamin, Anthony Msafiri, alishtuka saa 10.45 alfajiri na kusikia kelele za watu wakiomba msaada. “Kwanza nilifikiri tumevamiwa na majambazi, maana nilikuwa usingizini, lakini baada ya kuamka nilishuhudia nyumba zote zimejaa maji huku vitu vikielea, nilimkuta Mama Nyanjige - mama mzazi wa Stella aliyesombwa maji, akilia akiniomba kumwokoa Stella,” alisema Msafiri. “Nilichukua tochi na kufuatilia mkondo wa maji, nikawatoa baadhi ya watoto walionasa kwenye baadhi ya nyumba na kuelekea kambi ya Polisi Mabatini, ambako tulikutana na maaskari na tulipowauliza, wakasema Stella aliokolewa na mwanamke. “Alikuwa akielea huku akipiga kelele za kuomba msaada kwa maaskari hao, ndipo walipochungulia dirishani wakamwona na kuokolewa na mke wa askari,” alisema na kuongeza kuwa walimpeleka kituo cha afya na hatimaye hospitali ya mkoa ya Sekou Toure alikolazwa. Wakizungumza kwa uchungu mbele ya wananchi waliofurika eneo hilo, waathirika Issa Mauba, Tatu Ally na Hassan Babu, walidai kuwa chanzo cha mafuriko ya mara kwa mara Mabatini ni ujenzi usiozingatia mipango. Hii ni mara ya pili katika kipindi kifupi, Jiji la Mwanza kukumbwa na mafuriko huku ya hivi karibuni yakisababisha watu sita kupoteza maisha na zaidi ya 200 makazi. Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Wilson Kabwe, alisema tayari timu ya wataalamu imefika mitaa hiyo ya mafuriko ingawa hakukuwa na athari za kutisha. “Timu yangu ya wataalamu imefika maeneo yaliyopata mafuriko na tutatoa taarifa baadaye na tuone nini cha kufanya juu ya waathiriwa wa mafuriko, baada ya mvua ya jana,” alisema Kabwe.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote