Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, March 16, 2010

Trawu, wafanyakazi TRL kutoa tamko leo

CHAMA cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu) kitakutana na wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) ili kutoa tamko la pamoja baada ya serikali kutangaza azma ya kuchukua hisa za mwekezaji ambaye ni Rites ya India. Tamko hilo linakuja wakati zikiwa zimepita siku chache tangu serikali kutangaza azma hiyo ya kuchukua hisa zake ambazo ni asilimia 51 kutoka Rites ambayo ilitakiwa iwekeze dola 8 milioni za Kimarekani (sawa na zaidi ya Sh10 bilioni za Kitanzania) katika mkataba wake wa miaka 25 ulioanzia mwaka 2007. Katibu mkuu wa Trawu, Sylvester Rwegasira aliiambia Mwananchi jana kuwa hatua hiyo itaweka sawa suala hilo kutokana na wafanyakazi kuwa na mawazo tofauti tangu serikali itangaze azma hiyo. Kesho tutakutana na wafanyakazi ili kupata tamko la pamoja ambalo litakuwa limebeba mawazo na maoni ya wafanyakazi wote wa TRL hasa baada ya serikali kuamua kununua hisa, alisema Rwegazira. Kama kutakuwa na mabadiliko yeyote ya muda au chochote, tutafahamishana lakini ni lazima tukutane na kutoa tamko la pamoja. Tangu serikali itangaze azma yake, wafanyakazi wa TRL waliokuwa wakizungumza na vyombo vya habari walikuwa wakitoa maoni tofauti, hali ambayo Rwegasira alisema inatakiwa imalizwe kwa wafanyakazi wote kukutana. Ili serikali iachane na Rites haina budi kutoa taarifa ya miezi mitatu kwa kampuni hiyo inayomilikiwa na serikali ya India na itatakiwa imlipe mwekezaji huyo Sh54 bilioni kama fidia za gharama mbalimbali na matumizi ambayo kampuni hiyo iliingia wakati wa kipindi cha uwekezaji na fedha nyingine Sh56 milioni ambazo zinatakiwa zilipwe kwa kampuni binafsi ya ulinzi ya Ultimate Security. Rites imekuwa ikidai kuwa haistahili kubebeshwa lawama kutokana na TRL kushindwa kuendeshwa kwa ufanisi kwa kuwa serikali ndiyo iliyoshindwa kutekeleza wajibu wake kwenye mkataba. Mkurugenzi mtendaji wa TRL, Hundi Chaundhary aliwaambia waandishi wa habari mwaka jana kuwa serikali inashindwa kuwaeleza wananchi yaliyomo kwenye mkataba ndio maana kampuni hiyo kubwa ya uendeshaji wa huduma za reli inalaumiwa.
Chanzo: Mwananchi

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote