Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, March 17, 2010

Mchungaji adaiwa kuua mwanaye kwa kumuibia Sh. 50,000

Mchungaji wa Kanisa la African Inland Church (AIC), Jonathan Sabuni (60), Mkazi wa kijiji cha Kasamwa wilayani Geita, Mkoa wa Mwanza, ameua mwanaye Amos Jonathan (16), kwa kipigo kwa tuhuma za kumwibia Sh. 50,000. Marehemu Amos alikuwa anasoma darasa la saba katika Shule ya Msngi Nyampa. Inadaiwa kuwa siku mbili kabla ya kutenda ukatili huo, mtuhumiwa aliikusanya familia yake ya watu wanne na kuwataka waombe baada ya kupotea kwa fedha hizo alizokuwa amepanga kuzifanyia ukarabati wa nyumba ya familia. Mbali na marehemu, wanafamilia wengine ni Baraka Jonatan (18) anayesoma kidato cha pili na mkewe, Esther Jonatahan. Inadaiwa kuwa mchungaji huyo mkewe na kuwataka waombe kuhususiana na upotevu wa fedha hiyo iliyokuwa kwa ajili ya ukarabati wa nyumba ya familia. Imedaiwa kuwa Machi 13, siku mbili baada ya mtuhumiwa kutoa muda kwa marerehemu kurejesha fedha hiyo na kufanya Ibada maalum aliyowakutanisha wanafamilia baada ya marehemu kukiri kuwa ndiye aliyeiba fedha hizo na kuahidi kuzirejesha lakini hakufanya hivyo. Akizungumzia tukio hilo, Esther Jonathan, mama mzazi wa marehemu Amos alisema jana kuwa siku iliyofuata marehemu kwa woga aliamka alfajiri na kuondoka nyumbani kukwepa hasira ya baba yake lakini ilipofika saa nne alimtuma kaka yake Baraka kumrejesha nyumbani. Alisema wakiwa nyumbani saa tano ndipo mtuhumiwa alipoanza kumpiga marehemu kwa fimbo, rungu na mateke akidai marehemu alikuwa ameficha fedha hizo. Mama huyo alisema kuwa alijaribu kuingilia kati kumzuia mumewe kumpiga marehemu, lakini hakumsikiliza. Alisema ilipofika saa moja jioni marehemu alionekana kuzidiwa na ndipo mtuhumiwa alipoacha kumpiga na kwamba hali ya marehemu ilizorota ghafla na ilipofika saa 4:45 usiku mtuhuiwa alimwita Mchungaji Charles Mpanduji wa AIC kumuombea. Hata hivyo, kabla ya kumwita mchungaji mwenzake kumuombea marehemu, mtuhumiwa alimwosha marehemu mwili wote kumuondoalea uchafu kabla ya kukata roho. Kwa mujibu wa Ester, baada ya kugundua kuwa marehemu amekata roho, ndipo mtuhumiwa alipotoka nje na kisha kumuaga mkewe kuwa alikuwa anatoka kuelekea kusikojulikana, lakini yeye Ester) alimshtukia na kumzuia Kwa kumkaba shati asiondoke huku akipiga kelele kutaka msaada wa majirani, lakini baadaye alizidiwa nguvu na kumponyoka na ndipo mtuhumiwa alipotoroka. Kamanda wa Polsisi wa Mkoa wa Mwanza, Simon Sirro, alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote