Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, March 26, 2010

Vituko Mahakamani

Washtakiwa watatu wanaokabiliwa na kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha, jana walimmwagia kinyesi askari na kutoroka wakati wakiwa kwenye chumba cha mahabusu. Mahabusu hao walikimbia wakiwa uchi huku wakiwa wamejipaka kinyesi mwilini, kabla ya askari kuwakamata na kuwarudisha katika Mhakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam. Washtakiwa hao ambao waliachiwa huru baada ya Hakimu Richard Kabate wa Mahakama hiyo kuwaondolea shitaka hilo, walifikia hatua hiyo baada ya kuwekwa tena chini ya ulinzi na askari kwa ajili ya kurudishwa kituo cha polisi cha Magomeni kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka mengine mapya ya unyang'anyi wa kutumia silaha. Tukio hilo lilitokea mchana wakati askari wakijiandaa kuwatoa washtakiwa chumba cha mahabusu ili wawapandishe kwenye gari wawapeleke kituoni, ndipo washtakiwa walipotoroka wakiwa uchi. Katika sakata hilo, mmoja wa askari ambaye ni askari magereza mwenye namba A 7690 koplo Peter alimwagiwa kinyesi hicho kwenye sare yake na washtakiwa hao. Askari baada ya kuona hali hiyo walifyatua risasi hewani kuwatawanya watu waliokuwepo mahakamani ili wapate nafasi ya kuwafukuza washtakiwa ambao tayari walikuwa wakitokomea mitaani. Hata hivyo askari waliwakamata washtakiwa wawili, ambao walikuwa wakikimbia uchi eneo laKinondoni Bwawani, wakati mshtakiwa mmoja ambaye alikuwa na nguo alikamatwa na wananchi na kupata kipigo kabla ya askari kufika na kumchukua. Washtakiwa hao ambao walikuwa wamechoka kwa kipigo walichukuliwa kwenye gari la polisi lenye namba T213 AMV kupelekwa kituo cha polisi cha Magomeni kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka mapya. Washtakiwa hao waliotoroka ni Rashid Salum, (25), Hamza Abdallh (27) na Juma Mathis (24).

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote