Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, February 18, 2010

Asanteni Ufaransa

BALOZI wa Ufaransa nchini, Jacques de Labriolle, jana amekikabidhi msaada Chama Cha Msalaba Mwekundu tawi la Tanzania, wenye thamani ya takribani Sh milioni 100 za Tanzania kwa kuwasaidia waathirika wa mafuriko wilayani Kilosa katika mkoa wa Morogoro. Balozi Labriolle amesema, Serikali ya Ufaransa imetoa Euro 50,000 kuzisaidia zaidi ya familia 200 zilizokumbwa na mafuriko Kilosa. “Mwezi uliopita, mara moja baada ya maafa haya, Chama Cha Msalaba Mwekundu Ufaransa kimetuambia kwamba hali katika wilaya ya Kilosa ilikuwa mbaya sana na kimetupa ushauri kuitikia ombi la msaada wa dharura lililotolewa na Chama Cha Msalaba Mwekundu Tanzania” amesema Balozi huyo katika hotuba aliyoitoa kwa lugha ya Kiswahili. Amesema, fedha hizo zimetumika kununua vifaa vya kuwasaidia waathirika wa Kilosa, vikiwemo vyandarua, vyombo vya kupikia, mahema, dawa za kusafisha maji ya kunywa, na pia kugharamia usambazaji wa maji safi kwenye maeneo yaliyokumbwa na mafuriko.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote